Breaking News

Mar 10, 2016

KURUSHWA MAKOMBORA YA BALISTIKI YA IRANI ; SISITIZO LA KUIMARISHWA NGUVU YA KUZUIA MAKOSA YA ADUI

Kurushwa makombora ya balistiki ya Iran; sisitizo la kuimarishwa nguvu ya kuzuia makosa ya adui
Hivi Karibuni Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilirusha angani kwa mafanikio makombora kadhaa ya balistiki ikiwa ni katika kuyafanyia majaribio.
Luteka hiyo ya makombora ambayo inasisitiza udharura wa kuonyeshwa nguvu ya kuzuia kufanyika makosa ya adui na kujitayarisha Iran ya Kiislamu katika pande zote kwa ajili ya kukabiliana na kila aina ya vitisho dhidi ya Mapinduzi, Mfumo na ardhi yote ya Iran, imefanmyika katika hatua kadhaa. Kamanda mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran IRGC alisisitiza siku ya Jumanne mwishoni mwa luteka hiyo iliyopewa jina la "Nguvu ya Wilaya' kwamba kila mtu anayeifanyia uadui zaidi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran bila shaka ndiye anayepaswa kuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na uwezo na kujitayarisha Iran katika uwanja huo. Majaribio hayo ya makombora ya Iran yametajwa na baadhi ya watu kuwa tishio kwa usalama. Josh Earnest Msemaji wa White House katika matamshi yake ya kila siku mbele ya waandishi habari ameashiria Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) na kusema kuwa licha ya kuwa majaribio hayo hayakiuki mapatano ya mpango huo lakini serikali ya Washington inachunguza iwapo suala hilo linapasa kuchunguzwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa au la.
Peter Cook, Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani pia amesema kuwa majaribio hayo ya makombora ya Iran yanatia wasiwasi na kudai kuwa yanakiuka maazimio ya Baraza la Usalama.
Kwa mujibu wa azimio nambari 1929 lililopasishwa na Baraza la Usalama mwezi Juni 2010 Iran iliizuiwa kufanya majaribio yoyote ya makombora ya balistiki, lakini azimio jipya nambari 2231 lililopasishwa na baraza hilo mwezi Julai mwaka uliopita, baada ya kufikiwa mapatano ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1 mashuhuri kwa ufupisho wa JCPOA, maazimio yote ya hapo kabla ya baraza hilo dhidi ya Iran yalifutwa. Katika azimio hilo jipya Iran iliombwa kutotengeneza makombora yaliyo na uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia, katika kipindi cha utekelezaji wa mpango wa JCPOA. Hivi sasa inadaiwa kuwa makombora ya Iran yana uwezo wa kubeba vichwa vya aina mbili yaani vya kawaida na vya nyuklia. Hii ni katika hali ambayo Iran haina makombora yaliyotengenezwa kwa ajili ya kubeba vichwa vya nyuklia. Hata kabla ya kutiwa saini mapatano ya JCPOA, Iran ilitangaza wazi kwamba makombora ya kujilinda ya Iran si suiala linaloweza kujadiliwa na kwamba haijawahi kufanya mazungumzo na Marekani au upande wowote ule kuhusiana na kadhia hii. Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza wazi kupitia viongozi wake wa ngazi za juu kwamba silaha za nyuklia hazina nafasi katika mfumo wake wa ulinzi. Pia hakuna wakati wowote ambapo makombora ya Iran yametengenezwa kwa ajili ya kubeba vichwa vya nyuklia wala majario yoyote kufanyika katika uwanja huo. Kwa maelezo hayo, uwezo wa kujilinda wa makombora ya Iran si tu kwamba sio tishio kwa usalama wa wengine bali ni nguvu ya kuzuia maadui kufanya makosa ya kihujuma, na hilo ni kwa maslahi ya usalama wa eneo la Mashariki ya Kati na ulimwengu mzima kwa jumla. Ni wazi kuwa Wamarekani wanaeneza propaganda dhidi ya makombora ya Iran ili waweze kuendeleza mpango wao wa kuidhihirisha Iran kuwa tishio kwa usalama wa eneo. Marekani imekuwa ikitumia masuala matatu ya uwezo wa makombora ya Iran, haki za binadamu na demokrasia, kama visingizio vya kuzidisha mashinikizo dhidi ya Iran. Jambo hili linabainisha wazi kwamba Marekani ingali inatumia madai yasiyo na msingi ili kudumisha uadui wake wa muda mrefu dhidi ya Iran.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Pages