Breaking News

Your Ad Spot

Mar 10, 2016

'MGOGORO WA SYRIA UTATULIWE KWA KUHESHIMU UMOJA WA KITAIFA'

'Mgogoro wa Syria utatuliwe kwa kuheshimu umoja wa kitaifa'
Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayeshughulikia masuala ya Kiarabu na Kiafrika amesema kuwa,mgogoro wa Syria unapaswa kutatuliwa kwa kuheshimu ardhi yote, mamlaka na umoja wa kitaifa wa nchi hiyo ya Kiarabu.
Hossein Amir Abdollahiyan amesema hayo katika mazungumzo yake kwa njia ya simu na Staffan de Mistura mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria na kusisitiza juu ya udharura wa kutazama mambo kwa uhalisia wake katika kufuatilia suala la kupambana na ugaidi na mwenendo wa kisiasa katika nchi hiyo ya Kiarabu. Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayeshughulikia masuala ya Kiarabu na Kiafrika amesisitiza kuwa, kuna haja ya kuwa macho na hatua ambazo zinapelekea kuyaimarisha makundi ya kigaidi.
Kwa upande wake Staffan de Mistura mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria ameashiria katika mazungumzo yake na Hossein Amir Abdollahiyan juu ya nafasi muhimu na athirifu ya Iran katika kuupatia ufumbuzi wa kisiasa mgogoro wa Syria na kuelezea azma ya kweli ya Umoja wa Mataifa katika kufuatilia kadhia ya mgogoro wa nchi hiyo ya Kiarabu.
Wakati huo huo de Mistura amesema mazungumzo kuhusu Syria yanayotarajiwa kuanza Jumatatu huko Geneva, Uswisi hayataangazia masuala ya kibinadamu na sitisho la mapigano. Akizungumza na waandishi wa habari Jumatano baada ya mkutano wa kikundi cha kimataifa cha usaidizi wa Syria, ISSG, de Misturra amesema badala yake ajenda zitakuwa ni uongozi mpya, katiba na uchaguzi, yaani chaguzi zijazo katika miezi 18 ijayo za Rais na wabunge. Masuala ya sitisho la mapigano kinadharia na kivitendo tunaamini hayapaswi kujadiliwa kwenye mazungumzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages