Rais wa Marekani amejadidisha hali ya hatari kuhusu Iran. Ikulu ya
White House imetoa taarifa ikisema kuwa baada ya Barack Obama
kuidhinisha tena hali ya hatari ya kitaifa kuhusu Iran, mabunge ya
Kongres na Senate yatajulishwa rasmi kuhusu uamuzi huo.
Taarifa hiyo ambayo ilitolewa tarehe 9 Machi inasema: Pamoja na
kuwepo mapatano ya nyuklia, baadhi ya hatua na sera za serikali ya Iran
ni kinyume cha maslahi ya Marekani na hivyo Iran inahesabiwa kuwa tishio
lisilo la kawaida kwa usalama wa taifa, sera za kigeni na uchumi wa
Marekani. Kwa msingi huo kuna ulazima wa hali ya hatari kitaifa iendelee
kuwepo kuhusu Iran na baadhi ya vikwazo dhidi yake
"Sheria ya Hali ya Hatari ya Kiuchumi Kimataifa" ilipitishwa mwaka
1977 katika Bunge la Kongress ya Marekani. Kwa mujibu wa sheria hiyo,
rais wa Marekani anaweza kutangaza hali ya hatari ya kitaifa kufuatia
tishio lisilo la kawaida la kigeni kwa usalama wa Marekani.
Hatua zinazochukuliwa katika fremu ya uamuzi huo ni kama vile kuzuia
mabadilishano ya kibiashara, kufunga akaunti na kuzuia mali za nchi
inayolengwa.
Kwa kutegemea sheria hii, mwezi Machi mwaka 1995 rais wa wakati huo
wa Marekani, Bill Clinton alipasisha sheria ya hali ya hatari kuhusu
Iran. Sheria hiyo hujadidishwa kila mwaka.
Hatua hii mpya ya Ikulu ya White House ni dalili ya wazi kuwa, kwa
mtazamo wa Marekani, Iran bado ni tishio kwa nchi hiyo. Hii ni katika
hali ambayo tukiangazia historia ya uhasama wa Marekani katika kipindi
cha zaidi ya nusu karne iliyopita, itabainika wazi kuwa Marekani ndiyo
tishio kuu kwa usalama wa Iran.
Uhasama huo wa Marekani dhidi ya Iran ulianza hata kabla ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Hapa tunaweza kuashiria baadhi tu ya vitendo vya uhasama vya Marekani
dhidi ya Iran ambavyo ni pamoja na kupindiliwa serikali ya kisheria ya
Iran mwaka 1953 katika njama ya pamoja ya Marekani na Uingereza, kuunga
mkono makundi ya kigaidi, kuunga mkono uvamizi wa Saddam dhidi ya Iran
na kumhimiza kutumia silaha za kemikali na hatua ya meli ya kivita ya
Marekani ya kutungua kwa kombora ndege ya abiria ya Iran ikiwa na abiria
290 katika maji ya Iran katika Ghuba ya Uajemi mwaka 1988.
Baada ya kumalizika vita vya Saddam dhidi ya Iran, Marekani
iliendeleza uhasama wake wa kuiwekea Iran vikwazo vya kiuchumi sambamba
na kutoa vitisho dhidi ya nchi hii ili kuizuia isisitawi kiuchumi.
Aidha katika kipindi cha miaka 12 iliyopita, Marekani iliibua madai
yasiyo na msingi kuhusu Mapngo wa Nyuklia wa Iran na hivyo kuanzisha
duru mpya ya uhasama wake. Hivi sasa pia Marekani imeendeleza uhasama
huo kwa kuibua masuala kama vile wasi wasi kuhusu mpango wa makombora ya
kujihami ya Iran jambo ambalo halina uhusiano hata kidogo na mapatano
ya nyuklia ya Iran.
Marekani pia inatoa madai yasiyo na msingi kuwa eti Iran inaunga
mkono ugaidi. Hii ni katika hali ambayo dunia inafahamu kuwa Marekani
ndiyo iliyoibua kundi la kigaidi la Al Qaeda ili kufikia malengo yake
haramu katika eneo. Baada ya kundi hilo kuwa tishio kwa Marekani,
Washington ilitekeleza hujuma ya kijeshi dhidi ya Afganistan. Aidha kwa
kusingizio cha kulinda usalama wa Iraq, Marekani iliivamia na kuikalia
kwa mabavu nchi hiyo na matokeo yake yamekuwa ni kuibuka kundi la
kigaidi la ISIS au Daesh na mamia ya makundi mengine ya kigaidi duniani.
Aidha Marekani inaendeleza uungaji mkono wa nyuma ya pazia kwa makundi
hayo ya kigaidi kwa kutoa msaada kwa nchi kama Saudia inayolea magaidi.
Aidha kwa njia hiyo Marekani inaendeleza sera za chuki dhidi ya Iran
katika eneo.
Utambulisho wa kujadidishwa hali ya hatari kuhusu Iran ni sehemu ya
mkakati wa Marekani wa kuhalalisha sera zake zisizo za kimantiki na za
uhasama dhidi ya Iran. Kilicho wazi ni kuwa lengo la uchochezi wa sasa
wa Marekani ni kwa lengo la kufikia mkakati huo wa Washington.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269