Breaking News

Your Ad Spot

May 19, 2016

66 WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA BAADA YA NDEGE YA ABIRIA YA MISRI KUTOWEKA KWENYE RADA

Ndege ya abiria ya shirika la EgyptAir iliyokuwa imebea abiria 56 na wahudumu 10 wakiwemo marubani imetoweka kwenye rada, ikitokea mji mkuu wa Ufaransa Paris kuelekea Cairo, mji mkuu wa Misri.
Gazeti la serikali la Ahram limeripoti kuwa, ndege hiyo yenye nambari ya usajili A320, ilikuwa inaruka umbali wa mita 11,300 kabla ya kutoweka kwenye rada, mashariki mwa bahari ya Mediterranean, maili 10 kabla ya kuingia kwenye anga ya Misri. Maafisa wa Idara ya Safari za Anga nchini Misri wamesema yumkini ndege hiyo imeanguka katika bahari hiyo.
Kwa mujibu wa Wizara ya Uchukuzi ya Misri, abiria waliokuwa kwenye ndege hiyo ni pamoja na Wamisri 30, raia 15 wa Ufaransa na Muingereza mmoja.
Itakumbukuwa kuwa, ndege nyingine ya abiria ya shirika la Metrojet la Russia nambari A321, ilianguka katika Peninsula ya Sinai nchini Misri Oktoba 31 mwaka jana, na kuua watu wote 224 waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Aidha ndege nyingine ya abiria ya shirika la EgyptAir iliyokuwa na abiria 55 na wahudumu 7 ambayo ilikuwa inatoka Alexandria kwenda jijini Cairo, ilitekwa nyara na raia wa Misri ambaye aliaminika kuwa na akili taahira kwa jina Seifuddin Mustafa ambaye alidai kuwa alifanya hivyo ili kuishinikiza serikali ya Cairo iwaachie huru wafungwa wa kisiasa kabla ya kubadili kauli yake na kusema kuwa alitaka aletewe mtalaka wake raia wa Cyprus waonane katika uwanja wa ndege wa kisiwa hicho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages