Breaking News

Your Ad Spot

May 23, 2016

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO SAID MECKY SADICK AFANYA ZIARA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSGI, MUWASA

Mkuu wa Mko wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidick akiwa ameongozana na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) John Ndetico (mwenye tai) alipofanya ziara katika mamlaka hiyo .
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) John Ndetico akitoa taarifa ya Mamlaka hiyo kwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick alipotembelea ofisi za MUWSA.
Baadhi ya Viongozi wa Serikali pamoja na Wakuu idara katika Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakisikiliza kwa makini taarifa iliyokuwa ikitolewa.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na viongozi wengine wakiwa katika chanzo cha maji cha Nsere .
Chanzo cha Maji cha Nsere ambacho kiwango cha maji kinatajwa kushuka kutoka lita za ujazo Milioni 12 hadi Milioni 9.5.
Mkuu wa mkoa Saidi Mecky Sadick akitembelea maeneo ya chanzo hicho.
Mkuu wa Mkoa Said Mecky Sadick na viongozi wengine wakiwa katika chanzo cha maji cha Shiri 
Meneja ufundi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi(MUWSA) Mhandisi Patrick Kibasa akitoa maelezo ya chanz hicho kwa Mkuu wa mkoa Said Mecky Sadick na ujumbe wake.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadick na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya chanzo hicho.
Mkuu wa mkoa Said Mecky Sadick akitia saini katika kitabu cha wageni alipotembelea chanzo cha maji cha Shiri.
Mkuu wa Mko wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akitembelea kisima cha maji cha Mawenzi.
Kisima cha Maji cha Mawenzi.
Tani la Maji lililopo katika eneo la Kisima cha Mawenzi.
Mkuu wa Mkoa akiwa katika jengo la kuendeshea mitambo ya visima viwili vipya vya mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) vilivyopo eneo la KCMC.
Ujumbe wa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ukiwa katika moja ya visima vya zamani ambacho kinataraji kufanyiwa ukarabati.
Meneja Ufundi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) akitoa maelezo katika tanki la maji la Longuo ambalo litatumika kwa ajili ya kuhidhi maji yatakayotumika kwa wakazi wa Kiborironi na vijiji vya Korini na Kikarara.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages