Raila Odinga
Rais wa
Kenya Uhuru Kenyatta anafanya mazungumzo na kiongozi wa upinzani nchini
humo Raila Odinga ili kuondoa wasiwasi wakati ambapo taifa hlo
linajiandaa kwa uchaguzi mwaka mkuu ujao.
Bw Odinga
alikatiza ziara yake ya kushiriki katika mazishi kusini magharibi mwa
eneo la Natol ili kuhudhuria mkutano huo wa Uhuru Kenyatta katika mji
mkuu wa Nairobi.
''Nilipokea
simu kutoka ikulu ya mkutano na rais Uhuru Kenyatta.Naomba ruhusa yenu
watu wa Narok nielekee kuzungumza naye,alinukuliwa na gazeti la Daily
Nation akiwaambia waombolezaji.Nitatangaza kwa Wakenya iwapo
tumekubaliana na iwapo hatujakubaliana pia nitawaelezea'', aliongezea bw
Odinga.
Uhuru Kenyatta
Muungano
wa upinzani nchini Kenya Cord umeapa kuhudhuria mkutano jijni Nairobi
hapo kesho,licha ya kwamba serikali ilitangaza kupigwa marufuku.
Watu kadhaa wameuawa katika ghasia kati ya polisi na wafuasi wa upinzani wanaopigania mabadiliko ya sheria ya kupiga kura. BBC
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269