Breaking News

Your Ad Spot

May 15, 2016

USIKU WA DR. WILFRED LEKULE

Dr. Wilfred Lekule pichani (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Dr. Wilfred Lekule pichani katika pozi na mama Merina Lekule
Mshehereshaji katikati akiwa ameshika kisemeo,  akiwa katika picha ya pamoja na Wanatekinolojia ya Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili
Mkuu wa Skuli ya Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Dr. Elison Simon (wa kwanza Kushoto) akiwa na madaktari wenzake, wa kwanza kulia ni Mtaalamu wa Meno Dr. Joakim Nyerere,  wa tatu kulia ni Dr, Mandari na anae mfatia kushoto kwake ni mkewake Magdalena Mandari

Dr. Lekule akiingia Ukumbini na familia yake wakati wa hafla fupi ya kumuaga
Dr. Lekule aki cheza rumba la kwaito wakati wa hafla yake fupi ya kumuaga
Mmoja wa wataalamu hao, Duma, (wa tatu kulia) akiwa ni kivutio kwa kulisakata rumba la sebene la muziki wa kikongo wakati wa hafla ya kumuaga Dr, Lekule kwa mujibu wa sheria



Mtoto wa Dr. Lekule, Oscar Lekule ambae ni Mhandisi wa TCCL  akiwapungia Mikono wataalamu hao mara alipo tambulishwa wakati wa hafla fupi ya baba yake iliyofanyika Dar es Salaam


Dk. Gaudensia Mgoma, akitoa utambulisho na kuwashukuru wataalamu hao kujitoa kwa hali na mali kukamilisha hafla hiyo iliyofana



Mwenyekiti wa hafla hiyo, Ewald Nyaki (wakwanza kulia) akigonganisha Glas na meza kuu akiwemo mstaafu Dr, Lekule wapili kushoto, wapili kulia ni mama Lekule na wakwanza kushoto ni Oscar Lekule ambae ni Mhandisi wa TCCL  
Baadhi ya Madaktari wakipita meza kuu wakigonganisha glas









Mkuu wa Skuli ya Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Dr. Elison Simona (wapili kulia) akigongamisha glasi kwa pamoja na Mstaafu Dr. Lekule watatu kulia wa Madaktari wengine, wapili kushoto ni mama lekule

Fundi Sanifu Meno, Leonald Magea (kushoto) akimkabidhi Risala mara baada ya kuisoma katika hafla hiyo
Mkuu wa Skuli ya Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Dr. Elison Simon akizungumza jambo wakati wa hafla hiyo








































Khamisi Mussa

WAFANYAKAZI wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kitengo cha Tekinolijia ya meno, wamempongeza Dk. Wilfred Lekule kwa kufikia hatamu kwenye utumishi wa umma kisheria na kuwa mfano wa kuigwa kwao.

Akisoma hutuba kwa niaba ya wanafunzi wahimu wenzake waliwahi kufundishwa na Dk. Lekule, Fundi Sanifu Meno Leonald Magea,  alisema wakati wa utumishi wake wakati akiwa Mkuu wa Chuo cha Tekinolojia ya meno, licha ya kukutana na changamoto kadhaa lakini hakusita kutoa mchango wake kwa ajili ya kuendeleza taaluma hiyo chuoni hapo.

"Ulipokuwa Mkuu wa Chuo hiki, licha ya kukumbana na changamoto lukuki lakini hukisita katika utoaji wa elimu hapa chuoni hali iliyisaidia wanafunzi waliopitia hapa kupata elimu ambao kwa sasa wamekuwa wakiitumia katika kuhudumia jamii inayowazunguka katika sehemu zai kazi," alisema.

Aliongeza kuwa kutokana na jambo hilo bado wanaendelea kuthamini na kukumbuka mchango wa Dk. Lekule ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria na kukufanua kuwa wamehamasika kuandaa sherehe ya kumpongeza ili kukubali uwezo wake na mchango wake taaluma hiyo kwao.

Pia alisema licha ya kustaafu kwa Dk. Lekule katika utumishi wa Umma lakini bado mchango wake unahitajika katika kuihudumia jamii ipige hatua katika Tekinolijia ya meno ndani ya nchi na nje ya mipaka ya Tanzania.

Kwa niaba ya wenzake na kutambua mchango wake walimuomba Dk. Lekule kutosita kuendelea kutoa mchango wake kitaaluma kwa watu wa kada hiyo ambao bado wanahitaji msaada kutoka kwake licha ya kustaafu.

Pia Mkuu wa Chuo wa ambaye amepokea kijiti kutoka kwa Dk. Lekule, Dk. Gaudensia Mgoma aliahidi kufanya nyendo za mtangulizi wake kwa maana alikuwa kiungo muhimu baina ya wanachuo na jamii iliyopo chuoni hapo.

"Sitamwangusha na nimejifunza moyo wa uchapakazi, kwani wakati mwingine alikuwa akizidiwa na maradhi lakini alikuwa akifika chuoni na kupiga kazi hata mguu wake ulipokuwa umevimba haukumpa shida kutekeleza majukumu yake," alisema

mwisho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages