Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Ulemavu), Mhe.
Jenister Mhagama akizungumza na Wakurugenzi wa Mifuko ya Hifadhi za
Jamii kuhusu adhma ya utekelezaji wa agizo la ujenzi wa uchumi
unaotegemea viwanda. Kushoto ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe.
Mwigulu Nchemba na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe.
Charles Mwijage.
1.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Godius
Kahyarara (katikati) akizungumza katika kikao baina ya mifuho ya hifadhi
ya jamii na Serikali kilichozungumzia adhma ya utekelezaji wa agizo la
ujenzi wa uchumi unaotegemea viwanda. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PPF,
Bw. William Urio na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na
Udhibiti wa Sekta ya hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka.
Baadhi ya
wajumbe wa kikao cha mashauriano ya pamoja baina ya Serikali na Mifuko
ya Hifadhi ya Jamii kuhusu adhma ya ujenzi wa viwanda nchini
wakifuatilia kwa makini kikao hicho kilichoitishwa na Serikali kupitia
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Biashara na
Uwekezaji pamoja Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na
Ulemavu). Kikao hicho kilifanyika leo mjini Dodoma.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Godius Kahyarara
(katikati) akizungumza katika kikao baina ya mifuho ya hifadhi ya jamii
na Serikali kilichozungumzia adhma ya utekelezaji wa agizo la ujenzi wa
uchumi unaotegemea viwanda. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw.
William Urio na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na
Udhibiti wa Sekta ya hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka.
Jonas Kamaleki-Maelezo
Serikali
imekubaliana na mifuko ya hifadhi ya jamii kuanza utekelezaji wa ujenzi
wa viwanda nchini ili kuhakikisha kuwa adhma ya Tanzania ya kufikia
uchumi wa viwanda inafanikiwa ifikapo mwaka 2020.
Hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Rais John Pombe Magufuli aliyeitaka mifuko hiyo kuwekeza katika ujenzi wa viwanda nchini.
Akizungumza
mara baada ya kikao cha pamoja baina ya Serikali na mifuko hiyo, Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira, na
Ulemavu, Jenister Mhagama alisema Serikali imekusudia kuhakikisha
uanzishwaji wa viwanda unaanza haraka na kuongeza fursa za ajira nchini.
Mhagama
alisema kuwa mali ghafi na nguvu kazi ya kutosha zipo hapa nchini hivyo
hakuna sababu ya kuchelewa kuanza, ambapo Serikali imepanga hadi kufikia
mwishoni mwa mwaka 2016, utekelezaji wa adhma hiyo inaanza kuonekana
machoni mwa Watanzania.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa sekta ya
hifadhi ya Jamii (SSRA)alisema, Irene Isaka alisema ni agizo hilo
limekuja katika wakati mwafaka kwa kuzingatia kuwa kwa mifuko ya Hifadhi
ya jamii imekusudia kutekeleza kwa vitendo adhma ya Serikali ya awamu
ya tano inayosisitiza kuijenga Tanzania kupitia uchumi wa viwanda.
Kwa
mujibu wa Isaka alisema kuwa kanuni na mifumo ya mifuko hiyo inaruhusu
suala la uwekezaji katika viwanda ama kwa njia ya ubia au ya hati
fungani au kutoa mikopo kwa wanotaka kuwekeza katika viwanda.
Naye
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt, Adelhelm
Meru alisema uwekezaji katika viwanda ni suala ambalo linawashirikisha
wadau wengi zikiwemo wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ajili ya
malighafi za viwandani, Elimu kwa ajili ya ujuzi wa watu wa kufanya kazi
viwandani na Wizara ya Nishati na Madini kwa ajili ya nishati ya
kuendesha viwanda.
“Kwa
kuangalia raslimali tulizo nazo tumewaomba wadau waanze na viwanda
ambavyo vilikuwepo lakini kwa sasa havifanyi kazi kama vile Shirika la
Usagishaji la Taifa (NMC), General Tyre, NARCO na Kiwanda cha Viwadudu
cha Kibaha, alisema Dr. Meru na kuongeza kuwa malighafi za viwanda hivi
zinapatikana hapa nchini.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269