Pichani ni Mwenyekiti Mziwanda Chimwege ambae ametetea nafasi yake kwa kuibuka na kura 248 dhidi ya mpinzani wake Dr. wa watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili, Peter Kibacha kwa kupata kura 46. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Mwenyekiti huyo
nisiku mbili baada ya kuibuka mshindi nafasi ya Mwenyekiti wa Tawi la
Tughe Hospitali ya Taifa Muhimbili akipitia nyaraka mbalimbali ofisini kwake, ambapo mwenyekiti huyo anawashukuru wanachama wa tawi la hospitali ya Taifa Muhimbili kwakumpa heshma ya kuwaongoza kwa muda wa miaka mitano ijayo na anawaahidi kuwatumikia kwa busara, hekima, na maarifa yote, na mmoja wa mwanachama ambae hakupenda kutaja jina lake
, alisema hakuona haja ya kuchagua viongozi wengine kwa vigezo hao
wanafaa na ni wazoefu kwa kufahamu njia zote za kupita na anawaamini
niwachapakazi wazuri na kutetea haki za wafanyakazi bila woga
Katibu, Faustini Kaitaba akiwa ofisini akichapa kazi baada ya siku mbili ambapo amefanikiwa kutetea nafasi yake kwa miaka 5 kwa kura 215 dhidi ya mpinzani wake Peter Bokhe kwa kupata kura 91,
Wajumbe wakihakiki kura za mwenyekiti
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence
Museru (katikati) akiwa naviongozi wengine wakati wa zoezi la ufunguzi
wa Mkutano wa Viongozi wa Tawi la Tughe Hospitali ya Taifa Muhimbili,
kushoto ni Mkurugenzi Rasilimali watu, Makwaiya Makani na kulia ni Afisa Utumishi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Amos Hangaya
Baadhi
ya wanachama wa Tughe wa Hospiatli ya Taifa Muhimbili wakiwa tayari
kuchagua viongozi wapya watakao waongoza kwa kipindi cha miaka mitano
ijayo
Wajumbe wakiwa katika uchaguzi huo
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269