Na Masanja Mabula –Pemba
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba limewatoa hofu wananchi katika Mkoa huo wanaotekeleza ibada ya usiku wakati huu wa mfungo wa mwezi wa Ramadhan kwamba ulinzi umeirishwa .
Kamanda
wa Polisi Mkoa huo kamishna msaidizi mwandamizi , Hassan Nassir Ali
amesema , tayari kikosi cha usalama barabarani kimeongezwa nguvu kwa
kuongezewa watendaji ili waweze kuyafikia maeneo yote.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi Ofisini kwake ja ameahidi kuimarisha ulinzi
wa wananchi pamoja na mali zao kwa kipindi chote cha mfungo wa mwezi wa
Ramadhan kwa kuongeza maradufu doria za kawaida .
Aidha
ameeleza kuwa ulinzi umeiramishwa zaidi katika maeneo ya miji ya Wete ,
Konde na Micheweni na kuwatoa hofu wananchi wanaotekeleza ibada ya
usiku wakati huu wa mfungo wa mwezi wa Ramadhan .
Pia
Kamanda Hassan Nassir Ali amezidi kuwahakikishia wananchi kuwa
jeshi la Polisi litaendelea kutunza siri wanazozitoa na kuwataka kutoa
ushirikiano ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa .
“Napenda
kuwahakikishia wananchi kuwa jeshi la Polisi litaendelea kutunza siri
na taarifa ambazo wanazitoa , hivyo ni vyema kuendelea kutupa taarifa
ambazo zitafanikisha kuwadhibiti wanaopanga njama ya kufanya hujuma
”alifahamisha.
Amesema
utaratibu huo ulioandaliwa na Jeshi la Polisi umelenga kupunguza
matukio ya kihalifu pamoja na yale ya ukiukwaji wa kanuni na sheria za
nchi hususani za usalama barabarani .
Akizungumzia
tabia ya baadhi ya askari kuvujisha siri wanazopelekewa na raia wema ,
amesema kwamba ni vyema wananchi kuwasiliana moja kwa moja na wakuu wa
Vituo pamoja na maofisa wengine wa jeshi kuwaripoti askari wanaotoa siri
ili wachukuliwe hatua za kisheria .
“Ni
vyema wananchi kuwasiliana moja kwa moja na maofisa wa Jeshi la Polisi
kuwaripoti Askari ambao wanavujisha siri , kwani wanalipaka matope jeshi
na kwamba tutawachukulia hatua za kisheria ”alisisitiza.
Amesema
askari hao wanasababisha Jeshi kulaumiwa na wananchi , na kuwafanya
wananchi wakose imani na chombo chao cha ulinzi kutokana na askari
wachache wanaokiuka maadili ya kazi zao .
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269