Na
Mwandishi Maalum, New York
Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa
Mataifa, kuhusu masuala ya ugonjwa wa Ukimwi umeanza leo ( Jumatano)
hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania katika Mkutano huu wa siku tatu na ambazo umeandaliwa na Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa kwa Kushirikiana
na Shirika la Umoja wa Mataifa
linalohusika na Ukimwi ( UNAIDS),unaongozwa
na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dr. Hamis A Kigwangalla (Mb).
Wengine katika ujumbe ni Dr. Hamis H. Mwinyimvua Katibu Mkuu, Ofisi
ya Waziri Mkuu ( Policy &
Coordination), Mhe. Constantine John Kinyasu.
Mbunge wa Geita Mjini na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ukimwi, Dr.
Fatma Mrisho Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS
na wataalamu mbalimbali.
Akifungua mkutano huo, Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon amesema kunahatua kubwa zimefikiwa katika kukabiliana
na maambukizi ya virusi vya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi.
Ameyataja
baadhi ya mafanikio hayo ni pamoja na
ongeko la idadi ya watu wanapata
huduma za dawa za kuzuia makali ya ukimwi. Ongezeko hilo kwa mijibu wa Katibu Mkuu
limechangiwa na upatikanaji wa
dawa za gharama nafuu.
“Mpaka leo hii, zaidi ya
watu 17 milioni wanapatiwa huduma hiyo na hivyo kuokoa maisha ya mailioni ya
watu na wakati huo huo kuokoa mabilioni ya fedha.
Mafanikio mengine yametajwa kuwa ni
pamoja na kupungua wa maambukizo kwa asilimia
35 tangu mwaka 2000, kupungu kwa asilimia 43 ya vifo
vinavyohusiana na ugonjwa wa
ukimwi tangu mwaka 2003.
“ Ninayofuraha kwamba maambukizi mpya
ya virusi vinavyosababisha ukimwi kwa watoto yamepungua kwa asilimia 56 katika kipindi cha miaka kumi na
tano iliyopita. Ili hali nchi nne, cuba, Thailand, Armenia na Belarus hakuna kabisa maamkizo
kwa watoto. Ni matumani yangu tutakifia mahali pakuwa na sifuri ya
maambuki kwa watoto” akasisitiza Ban Ki
Moon.
Pamoja na mafanikio hayo yote, Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa, ametahadharisha kwamba
kama jumuiya ya kimataifa
haitatumia mafaniko hayo kuongeza kasi zaidi na kushughulikia tatizo
la ukimwi kwa nguvu zaidi kunauwezekano
mkubwa kwamba ugonjwa huo ukarudi kwa
kasi kubwa zaidi kulivyo ilivyo sasa na hususani katika nchi
zenye uchumi mdogo na wakati.
Viongozi wengine waliozungumza wakati
wa ufunguzi ni pamoja na Rais wa Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw Monges
Lykketoft na Mkurugenzi Mkuu wa UNAIDS Michael
Sidibe.
Katika siku hii ya kwanza ya mkutano wa kilele kuhusu Ukimwi, wajumbe kutoka karibu mataifa yote duniani
ambayo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa,
walipitisha tamko la kisiasa
kuhusu matokeo ya mkutano huu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269