Breaking News

Your Ad Spot

Jun 9, 2016

NAIBU WAZIRI WA AFYA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA UKIMWI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dk. Hamis Kigwangalla ( Mb)  akiwa na   baadhi ya wajumbe wa Tanzania Dk. Hamis Mwinyimvua, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Policy & Coordination)  na Constantine Kanyasu ambaye ni Mbunge wa Geita na Makamu  Mwenyekiti wa  Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi,  katika  siku ya kwanza ya  ufunguzi wa  mkutano wa ngazi ya juu  kuhusu Ukimwi ambao uluoandaliwa na  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kufungukiwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban Ki Moon   
Na  Mwandishi Maalum, New York
Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa Mataifa,  kuhusu masuala ya   ugonjwa wa Ukimwi umeanza leo ( Jumatano) hapa Makao  Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano huu wa  siku   tatu na ambazo umeandaliwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  kwa Kushirikiana na  Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na  Ukimwi ( UNAIDS),unaongozwa na  Naibu Waziri wa Afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Mhe. Dr. Hamis A Kigwangalla (Mb).
Wengine katika ujumbe ni  Dr. Hamis H. Mwinyimvua Katibu Mkuu, Ofisi ya  Waziri Mkuu ( Policy & Coordination), Mhe. Constantine John Kinyasu.  Mbunge wa Geita Mjini na   Makamu  Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ukimwi, Dr. Fatma Mrisho Mkurugenzi Mtendaji  wa TACAIDS na wataalamu mbalimbali.

Akifungua  mkutano huo,   Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban  Ki Moon amesema  kunahatua kubwa zimefikiwa katika kukabiliana na maambukizi ya virusi  vya  ukimwi na ugonjwa wa ukimwi.

 Ameyataja  baadhi ya mafanikio hayo ni pamoja na  ongeko la idadi ya  watu wanapata huduma za dawa za kuzuia  makali ya  ukimwi. Ongezeko hilo kwa mijibu wa   Katibu Mkuu  limechangiwa na upatikanaji wa  dawa za gharama nafuu.

“Mpaka leo hii,  zaidi ya  watu 17 milioni  wanapatiwa  huduma hiyo na hivyo kuokoa maisha ya  mailioni ya  watu  na  wakati huo huo kuokoa mabilioni ya fedha.
Mafanikio mengine yametajwa kuwa ni pamoja na kupungua wa  maambukizo kwa asilimia 35 tangu mwaka 2000,  kupungu kwa  asilimia 43 ya  vifo  vinavyohusiana na  ugonjwa wa ukimwi tangu  mwaka 2003.

“ Ninayofuraha kwamba maambukizi mpya ya  virusi vinavyosababisha ukimwi  kwa watoto yamepungua kwa  asilimia 56 katika kipindi cha miaka kumi na tano iliyopita. Ili hali nchi nne, cuba, Thailand,  Armenia na Belarus hakuna kabisa maamkizo kwa  watoto. Ni matumani  yangu tutakifia mahali pakuwa na sifuri ya maambuki  kwa watoto” akasisitiza Ban Ki Moon.

Pamoja na  mafanikio hayo yote, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  ametahadharisha kwamba kama  jumuiya ya kimataifa haitatumia  mafaniko hayo  kuongeza kasi zaidi na kushughulikia tatizo la ukimwi kwa  nguvu zaidi  kunauwezekano  mkubwa kwamba ugonjwa huo ukarudi kwa  kasi  kubwa zaidi kulivyo  ilivyo sasa na hususani katika nchi zenye  uchumi mdogo na wakati.

Viongozi wengine waliozungumza wakati wa ufunguzi ni  pamoja na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa, Bw Monges Lykketoft na Mkurugenzi Mkuu wa UNAIDS Michael  Sidibe.

Katika siku hii ya kwanza ya  mkutano wa kilele kuhusu Ukimwi,  wajumbe kutoka karibu mataifa yote duniani ambayo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa,  walipitisha tamko la  kisiasa kuhusu  matokeo ya mkutano huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages