Breaking News

Your Ad Spot

Aug 9, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWA MBOGO, NI BAADA YA KUBAINI UBADHIRIFU WA FEDHA UJENZI WA SOKO LA MWANJELWA, MBEYA



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia wananchi baada ya kufanya ukaguzi wa soko la Kimataifa la Mwanjelwa mkoani Mbeya leo Agosti 9, 2016 ambapo pamoja na mambo mengine amemuagiza Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, (CAG), afanye ukaguzi wa gharama za ujenzi wa soko hilo mara moja. (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

NA MWANDISHI MAALUM
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenda kufanya ukaguzi maalumu katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya baada ya kuwepo kwa ubadhilifu katika ujenzi wa soko la Kimataifa la Mwanjelwa.


Waziri Mkuu ametoa maagizo hay oleo hii Agosti 9, 2016 baada ya kulikagua soko hilo na kuzungumza na wanancvhi ambapo alisikitishwa na kiasi kikubwa cha fedha kilichotumika kujenga soko hilo.
 “Naambiwa ujenzi wa soko hili umegharibu shilingi Bilioni 26 badala ya zile zilizotengwa awali shilingi Bilioni 16, nah ii ni kutokana na uzembe uzembe tu, hii haikubaliki,” alifoka Waziri Mkuu.
Na wote watakaobainika kufuja fedha hizi watachukuliwahatua mara moja, alisema Waziri Muu Majaliwa ambaye alifuatana na mkewe Marry.
Hali kadhalika fedha shilingi milioni 489 zilizotolewana benki ya CRDB ili kuliendeleza soko hilo, matumizi yake hayaeleweki na hazijulikanizilifanya kitu gani na kumuagiza mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla kufanya uchunguzi ndani ya siku tatu na kumpagtia majibu.
  (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua soko hilo
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua soko hilo
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua soko hilo
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua soko hilo
 Waziri Mkuu akihutubia wananchi mara baada ya kutembelea soko hilo la kisasa

  Waziri Mkuu akihutubia wananchi mara baada ya kutembelea soko hilo la kisasa


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary  wakiagana na viongozi wa serikali  kabla ya kuondoka kwenye uwanja wa  ndege wa Songwe Mbeya  kurejea Dar es salaam Agosti 9, 2016. Kulia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Harrison Mwakyembe na  wapili kulia ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa Zelote Stephene.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages