Breaking News

Your Ad Spot

Sep 1, 2016

IRAN: UJENZI WA VINU VIPYA VYA NYUKLIA KUANZA MWEZI HUU NCHINI

Dk Ali Akbar Salehi, Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Ira
Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran amesema kuwa ujenzi wa vinu viwli vipya vya nishati ya nyuklia utaanza katika mji wa Bushehr kusini mwa Iran tarehe kumi mwezi huu wa Septemba.
Ali Akbar Salehi amesema kuwa, mapipa milioni 22 ya mafuta yataokolewa kila mwaka hapa Iran baada ya kujengwa vinu hivyo vya nyuklia.
Salehi amebainisha kuwa ujenzi wa vinu hivyo viwili vya nyuklia unatabiriwa kuchukua muda wa miaka kumi na kwamba mradi huo utagharimu dola bilioni kumi za Kimarekani.
Kinu cha nyuklia cha Bushehr kusini mwa Iran kilichojengwa kwa ushirikiano wa Iran na Russia
Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Nyuklia ya Iran pia amesema, Tehran itashirikiana na Russia kwenye ujenzi huo na kueleza kuwa mkataba huo umefikiwa kwa kuzingatia kushirikishwa vilivyo kiufundi viwanda vya ndani ya Iran katika utekelezaji wa mradi huo. 
Ali Akbar Salehi ameashiria uwezo wa Iran katika sekta ya nishati ya nyuklia na kubainisha kuwa, Tehran itakuwa na nafasi muhimu sana katika sekta ya nyuklia kwenye kipindi cha miaka kumi ijayo kwa kuzingatia mahitaji ya nchi katika kulinda na kudhamini maslahi ya wananchi hususan katika nyanja za nishati, viwanda, kilimo na tiba.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages