Breaking News

Your Ad Spot

Sep 11, 2016

MLIMBWENDE WA OZONA MISS LAKE ZONE 2016 APATIKANA

 
Jumamosi Septemba 10, 2016 kuamkia leo jumapili, kinyang'anyiro kikali cha kumsaka mlimbwende wa Kanda ya Ziwa, (OZONA MISS LAKE ZONE 2016), kimefanyika ambapo Mlimbwende, Eluminatha Dominick (pichani) kutoka mkoani Geita ameibuka mshindi miongoni mwa walimbwende 17 (baada ya mmoja kujitoa) waliokuwa wakiwania taji hilo.

Ushindi wa mlimbwende huyo ulionekana kuwafurahisha mamia ya watu waliohudhuria kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye Viunga vya Rock City Mall Jijini Mwanza, likiwa nimeandaliwa na kampuni ya Flora Talent Promotions chini ya Mkurugenzi wake, Flora Lauwo na kudhaminiwa na makampuni mbalimbali ikiwemo mdhamini mkuu, kampuni ya vipodozi ya OZONA pamoja na 102.5 Lake Fm Mwanza.

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Mhe.Jeseph Linzwa Kasheku Msukuma, alisema ni furaha kubwa mkoa wa Geita kunyakua taji la Ozona Miss Lake Zone 2016 na kwamba matarajio ni kujiandaa vyema kwa ajili ya kunyakua taji la Miss Tanzania 2016 ikiwa ni sawa sawa na matarajio aliyoyaeleza mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016.
Na BMG
Mlimbwende, Eluminatha Dominick (pichani) kutoka mkoani Geita ameibuka mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, miongoni mwa walimbwende 17 waliokuwa wakiwania taji hilo.
Mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (katikati) kutoka mkoani Geita. Mshindi wa pili ni Mery Peter (Miss Mwanza 2016, kushoto) na Mshindi wa tatu ni Lucy Michael (Geita, kulia).
Mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (katikati) kutoka mkoani Geita. Mshindi wa pili ni Mery Peter (Miss Mwanza 2016, kushoto) na Mshindi wa tatu ni Lucy Michael (Geita, kulia).
Aliyekuwa akishikilia taji la Miss Lake Zone
Aliyekuwa Miss Lake Zone (kulia), akikabidhi taji la Miss Lake Zone mpya (kushoto)
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaa ya Nyamagana, Mhe.Mary Tesha (kushoto) akimkabidhi mshindi wa Ozona Miss Lake Zone mfano wa ufunguo wa gari alilokabidhiwa kama zawadi. Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone amewazadiwa gari lenye thamani ya shilingi Milioni 12 na kampuni ya Ozona.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha, Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick, Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ozona, Dr.Thobias Mkina, wakiwa katika picha ya pamoja.
Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (kushoto) akiwa katika picha na Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma (kulia).
Washiriki walioingia nafasi tano bora ni, Eluminatha Dominick (wa pili kushoto kutoka Geita), Mery Peter (wa tatu kushoto kutoka Mwanza, Lucy Michael (wa kwanza kushoto kutoka Geita), Rose Masanja (wa pili kushoto kutoka Shinyanga) na Farida Hassan (wa kwanza kulia kutoka Mara).
Washiriki 17 wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Ozona Miss Lake Zone akizungumza na Wanahabari baada ya kukabidhiwa gari
Mchekeshaji Eric Omond kutoka nchini Kenya akizungumza na Vesterjtz wa BMG baada ya show
Kushoto ni Christian Bella, akizungumza na Vesterjtz wa BMG baada ya kudondoka burudani kali
Katikati ni mbunge Joseph Msukuma akizungumza na BMG
Kulia ni mmoja wa wanakamati akihojiwa na BMG
George Binagi-GB Pazzo (ushoto) katika picha ya pamoja na Christian Bella (kulia) baada ya show
Mwanahabari Sadam Sadick (kulia) akishow love na Bella
Ozona Miss Lake Zone 2016 (kushoto) akiwa na Vesterjtz
Kijukuu kutoka RFA akiwa na Ozona Miss Lake Zone 2016
Mambo ya karanga fotooo na Ozona Miss Lake Zone 2016

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages