Breaking News

Your Ad Spot

Sep 11, 2016

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUONGOZA IBADA YA KUWAAGA WALIOFARIKI KWENYE TETEMEKO BUKOBA

 Askofu msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Kanisa Katoliki, Methodius Kilaini, akibariki leo Septemba 11, 2016, majeneza 16 yaliyobeba miili ya watu waliofariki kutokana na madhara ya tetemeko la ardhi lililokumba mji wa Bukoba mkoani Kagera Septemba 10, 2016. Watu 16 wameripotiwa kupoteza maisha hadi hivi sasa.
 Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Kanisa Katoliki, Methodius Kilaini, akiongoza ibada hiyo
 Waziri Mkuu kassim Majaliwa akiwasili kwenye uwanja wa michezo wa Kaitaba alasiri hii Septemba 11, 2016 kuongoza ibada ya kuaga miili ya watu 16 waliofariki kwenye tetemeko hilo
 Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Kanisa Katoliki, Methodius Kilaini, akiongoza ibada hiyo
 Majeneza ya watu waliouawa kwenye tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Septemba 10, 2016, yakiwa yamepangwa kwenye uwanja wa michezo wa Kaitaba mjini Bukoba leo Septemba 11, 2016 tayari kwa i bada ya kuwaaga itakayoongozwa na waziri mkuu Kassim Majaliwa muda mfupi ujao. Watu 16 wameripotiwa kufariki dunia hadi leo hii kutokana na tetemeko hilo lililokumba maeneo yanayozunguka ziwa Victoria ambapo Manispaa ya Bukoba ndiyo iliyoathirika zaidi.
 Wataalamu wa jiolojia wa Marekani wanasema tetemeko hilo lenye ukubwa wa kipimo cha Richa 5.7 na lililokwenda umbali wa kilomita 10 chini ya ardhi, limezikumba nchi za Uganda na Rwanda. Mkuu wa wilaya ya Bukoba Deodatus Kinawilo, amesema watu 200 wanapatiwa matibabu kwenye hospitali ya rufaa ya Bukoba.
 Waombolezaji wakiwa kwenye uwanja wa Kaitaba tayari kwa ibada hiyo
  Waombolezaji wakiwa kwenye uwanja wa Kaitaba tayari kwa ibada hiyo
  Waombolezaji wakiwa kwenye uwanja wa Kaitaba tayari kwa ibada hiyo
 Baadhi ya majeruhi wakisubiri kupatiwa huduma kwenye hpspitali ya rufaa ya Bukoba Septembe 10, 2016.
Hii ni moja kati ya nyumba kadhaa zilizobomolewa kutokana na kishindo cha tetemeko hilo. (PICHA NA FAUSTINE RUTA)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages