Breaking News

Your Ad Spot

Oct 2, 2016

RAIS DK. MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI MPYA BODI YA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA-NIC, LEO

Rais  Dk. Magufuli
Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, leo tarehe 02 Oktoba, 2016 amemteua Laston Thomas Msongole kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Bima la Taifa (NIC).

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es Salaam, imesema  Laston Thomas Msongole anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Edmund Mndolwa ambaye amemaliza muda wake.

"Uteuzi wa Laston Thomas Msongole umeanza leo tarehe 02 Oktoba, 2016", imesema taarifa hiyo ya Ikulu iliyosaininiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, GersonMsigwa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages