Mkuu wa Idara ya Tiba wa hospitali hiyo, Dk. Olivia Rusizoka akitoa neno la ukaribisho kwa waalikwa baada ya kufungua kwa Sala maalum katika hafla hiyo
Mkurugenzi
wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dr, Hedwiga Swai akifungua
rasmi hafla hiyo wa kuwaaga wafanyakazi 4 waliostaafu kwa mujibu wa
Sheria
Waalikwa
Baadhi ya wakuu wa idara na waalikwa
Baadhi wa waalikwa ambani wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili
Wafanyakazi wakionyesha umahiri wao kwa kucheza wakati wa hafla fupi ya
kuwaaga wastaafu 4 waliomaliza muda wao kwa mujibu wa Sheria ya Tanzania
ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili (MNH)
Profesa Lawrence Museru
Mkuu
wa Idara ya Uuguzi na Mazingira ya Ndani Hospitali ya Taifa Muhimbili
(MNH), Zuhura Mawona (kushoto) akiomba Dua wakati wa kupata chakula cha
jioni kilicho andaliwa na kulia ni Mkuu wa Idara ya Tiba wa hospitali hiyo, Dk. Olivia Rusizoka
Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru
(kushoto) akikabidhiwa zawadi na wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MNH) kwa kupongezwa kwa kuthibitishwa kwake na Rais John
Pombe Makufuli wakati wa hafla ya kuwaaga wafanyakazi 4 waliostaafu kwa
mujibu wa sheria
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wameahidi kutoa ushirikiano kwa Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru baada ya kudhibitishwa na Rais Dk. John Magufuli.
Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wameahidi kutoa ushirikiano kwa Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru baada ya kudhibitishwa na Rais Dk. John Magufuli.
Kauli
hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na Daktari Bingwa
wa Kisukari wa hospitali hiyo, Dk. Wolfgang Bernard katika hafla ya
Wakuu wa idara ya Tiba wakati wa kuwaaga wafanyakazi wa MNH wanne
waliostaafu kwa mujibu wa Sheria.
Alisema
wanamshukuru Rais Magufuli kwa kumthibitisha Prof. Museru na kumuombea
dua, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kasim
Majaliwa na viongozi wote walioshiriki kufanya uamuzi huo.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Idara ya Tiba wa hospitali hiyo, Dk. Olivia
Rusizoka kwa niaba ya wafanyakazi wote alimshuru Rais Magufuli kwa
kumthibitisha Profesa Museru .
Rusizoka alisema kuwa wamejipanga kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkurugenzi huyo ili kufanikisha shughuli za kiutendaji hospitalini hapo.
"Sisi wafanyakazi wote tunamshukuru sana Rais wetu kutokana na kazi kubwa anayoifanya ya kuijenga nchi yetu, kikubwa kwetu ni kumuombea Dua kwa Mungu ili awe na maisha marefu yeye na wasaidizi wake wawe na afya njema wao na familia zao pia tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkurugenzi aliyemteua," alisema.
Rusizoka alisema kuwa wamejipanga kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkurugenzi huyo ili kufanikisha shughuli za kiutendaji hospitalini hapo.
"Sisi wafanyakazi wote tunamshukuru sana Rais wetu kutokana na kazi kubwa anayoifanya ya kuijenga nchi yetu, kikubwa kwetu ni kumuombea Dua kwa Mungu ili awe na maisha marefu yeye na wasaidizi wake wawe na afya njema wao na familia zao pia tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkurugenzi aliyemteua," alisema.
Museru kabla ya kuteuliwa kwake kuiongoza Hospitali ya
Taifa Muhimbili alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili MOI na kustaafu na ndipo Rais akamteua kukaimu nafasi hiyo na
hivi karibuni alimthibitisha.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269