Breaking News

Your Ad Spot

Oct 3, 2016

WANACHAMA 80 WA KUNDI LA DAESH WAUAWA LIBYA

Jeshi la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya limetangaza kuwa, limefanikiwa kuwaangamiza wanachama 80 wa kundi la kigaidi la Daesh katika mapigano yaliyotokea kwenye mji wa pwani wa Sirte.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya imesema kuwa, jeshi hilo limefanikiwa kuwaangamiza wanachama wasiopungua 80 wa kundi la kigaidi la Daesh waliokuwa wakitoroka kutoka eneo moja la mji wa Sirte. Taarifa hiyo imesema askari wasiopungua 8 wa Libya pia wameuawa katika mapigano hayo na wengine 57 wamejeruhiwa.
Jeshi la Libya likipambana na wanachama wa Daesh
Tarehe 12 Mei jeshi la Libya lilianza operesheli kubwa iliyopewa jina la al Bunyanul Marsus kwa shabaha ya kukomboa mji wa Sirte unaodhibitiwa na kundi la Daesh. Wanachama wa kundi hilo waliukalia kwa mabavu mji huo wa kaskazini mwa Libya mwezi Juni mwaka 2015.
Ripoti za hospitali za mji wa Sirte zinasema kuwa, zaidi ya askari 450 wanaoiunga mkono Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya na wanachama 2500 wa kundi la Daesh wamekwishauawa hadi sasa katika operesheni hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages