Na Magreth Magosso, Kigoma
IMEFAHAMIKA kuwa,Serikali ya awamu ya tano ya Rais John
Magufuli imedhamiria kuwekeza kwa dhati katika sekta ya afya ili kukabiliana na
changamoto ya uhaba wa vifaa na vifaa tiba ili kuzuia vifo vinavyozuilika ndani ya miaka mitano.
Akithibitisha kauli hiyo jana kigoma ujiji katika mkutano
mkuu wa wauguzi nchini waziri mwenye
dhamana Ummy Mwalimu alisema mpaka sasa wizara imepunguza baadhi ya kero za
vifaa akitolea mfano Hospitali ya taifa ya rufani ya Muhimbili ambapo
kunamabadiliko ya utenadaji kazi kwa watumishi wa afya.
“mimi ni mwanamke nipo kwa ajili ya wanawake wajawazito
katika kutaua kero zinazowakabili lakini msilalamike sana pale muuguzi
anapohitaji mipira ya mikono kwa kuwa kuna wakati vituo vya afya na hospitali
zetu hazina vifaa na vifaa tiba ,mchangie pale panapohitajika” alifafanua
Mwalimu.
Alisema ili kukabiliana na hilo serikali imetenga fedha za
kutosha kupunguza kero mtambukwa katika hospitali na vituo vya afya na zahanati
kulingana na bajeti husika lakini serikali ina dhamira ya dhati kupunguza vifo
vitokanavyo na uzazi,ili kuokoa uhai wa mama na mtoto.
Mwalimu alisema mpaka sasa mafanikio kwa baadhi ya magonjwa
yameonekana hasa ugonjwa wa ukosefu wa kinga mwilini (UKIMWI), Maralia, lakini
bado serikali inafanya jitihada za nguvu kuwekeza katika vifaa na vifaa tiba
kwa miaka mitano kwa nia ya kuimarisha uchumi wa taifa hasa rasilimali watu
ambao ni nguvu kazi ya taifa.
Aidha aligusia changamoto ya uhaba wa wauguzi nchini inakabiliwa kwa 48% hali
inayomlazimu kila muguzi kuhudumia wagonjwa 1500 kwa siku ambapo kwa mujibu wa
shirika la afya duniani (WHO) ilitoa mwongozo wa kuwa muguzi mmoja ahudumie
wagonjwa 8 kwa siku, ili kuwapunguzia mchoko wa kazi.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi Ummy Mwalimu Mkuu wa mkoa wa
kigoma, Emanuel Maganga alisema kada ya uguzi ni sehemu ya maisha ya
watu, serikali haina budi kutimiza mikakati yake katika kada hiyo, ambayo
inakabiliwa na changamoto kadhaa ambapo zikitiliwa mkazo ustawi wa jamii
utaimarika.
Mwisho.
--
Jamboleo news paper
0757736863
0757736863
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269