NA
MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA.
RAI
imetolewa
kwa wanawake wajawazito wasitumie dawa za asili za kuongeza uchungu katika
harakati za kujifungua kwa kuwa inahatarisha uhai wa mama na mtoto
,badala yake wafike mapema katika vituo vya afya ili kuokoa maisha yao.
Akitoa rai hiyo mbele ya ripota wa blog hii daktari
mfawidhi wa kituo cha Afya cha Nguruka Dkt. Stanford- Chamgeni, kwa
niaba ya mkuu wa wilaya ya Halmashauri ya Uvinza Mwamvua-Mrindoko
wakati akikabidhiwa jengo la wazazi (maternity ward,) katika kijiji cha mganza
kata ya mganza wilayani Uvinza, ambalo limetolewa na Kanisa la POOL
OF SILOAM.
Naye Kuhani Israel –Extra-Power, ambaye ni
mwakilishi wa kiongozi mkuu wa kanisa hilo, alisema hatua hiyo ni
sehemu ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kukamilisha huduma za
kijamii hasa kuokoa maisha ya mama mjamzito na mtoto.
Kuhani Power, aliongeza kwa kusema kuwa,
kusaidia maisha ya wenye uhitaji, lazima kuwepo na umoja kwa viongozi na jamii
kwa ujumla kwa kuwa Mungu hana upendeleo, kama kanisa nilazima itoe
huduma kwa jamii.
Kwa upande wake,Ofisa mtendaji wa kata ya Mganza
Bonifasi-Bahingai, amelishukuru kanisa hilo kwa kuwa wodi hiyo, itasaidia
kutatua changamoto ya uhaba uliokuwa ukikikabili kituo hicho na
kutoa wito kwa taasisi zingine za kidini kuona umuhim wa kusaidia huduma katika
jamii.
mmoja wa wananchi wa kijiji hicho, Dafroza Gwimo
alitanabaisha kuwa, uwepo wa wodi hiyo itawarahisishia
kuondoa changamoto iliyokuwepo ya kwenda kujifungulia mbali,
na kupelekea kuhatarisha maisha ya mama mjamzito na mtoto.
Mwisho,
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269