Breaking News

Your Ad Spot

Nov 26, 2016

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AZINDUA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI KANDA YA KASKAZINI

Uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini ulitanguliwa na maandamano yaliyopita katika barabara mbalimbali za mji wa Moshi na kuhitimishwa katika viwanja vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.
Washiriki kutoka Asasi mbalimbali wakipita mbele na mabango yakiwa na ujumbe mbalimbali katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini.
Baadhi ya viongozi wa taasisi mablimbali wakiwa wameketi meza kuu na mgeni rasmi wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya kaskazini Said Mecky Sadiki.
Mwenyekiti wa Kamati ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia,Elizabeth Mushi akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatli wa kijinsia.
Mwenyekiti wa Kamati ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Elizabeth Mushi akipeana mkono na Mgeni rasmi katika unzinduzi huo,Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadiki mara baada ya kutoa taarifa juu ya ukatili.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiki kutoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupina ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadiki akizungumza wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ,uzinduzi iliofanyika katika viwanja wa vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi katika Shule ya Polisi Theresia Nyangasa  akisoma taarifa juu ya vitendo vya kuutali na njia zilizoanza kuchukuliwa katika kukabiliana navyo wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya Kaskazini .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadiki pamoja na Mkuu wa wilaya ya Moshi Kippi Warioba wakifuatilia taarifa juu ya ukatili wa kijinsia iliyokuwa ikitolewa na viongozi wa Asasi mbalimbali .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akitoa cheti kwa Kaimu Kamnada wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Koka Moita cha kutambua mchango wa jeshi la Polisi katika kupamban vita dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadiki akipena mkono kabla ya kumkabidhi cheti Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake (TPF Network) Grace Lyimo ,kutambua mchango wake katika vita dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadiki akipeana mkono na Mwenyekiti wa Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi wilaya ya Moshi,Elina Maro kabla ya kumkabidhi cheti kutambua mchango wake katika vita dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akipata maelezo kutoka kwa baadhi ya washiriki alipopita kugagua mabanda ya maonesho ya shughuli zinazofanywa na taaisisi zinazopambana na ukatili wa kijinsia.
Mwenyekiti wa TAWREF ,Dafrosa Itemba akitoa taarifa juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kanda ya kaskazini uliofanyika katika viwanja vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages