Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya zimelaani shambulizi la kigaidi lililotokea katika soko la mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Taarifa iliyotolewa na Michael Keating, mwakilishi wa Umoja wa
Mataifa nchini Somalia imelaani vikali shambulizi lililolilenga soko la
mji Mogadishu na imewataka askari wa serikali kuwabaini wahusika wa
hujuma hiyo na kuwafikisha mahakamani.
Umoja wa Ulaya pia imelaani hujuma hiyo iliyoua raia kadhaa mjini
Mogadishu na kutangaza azma yake ya kufanya juhudi kubwa kwa ajili ya
kudhamini usalama wa taifa hilo la Pembe ya Afrika.
Mripuko wa bomu la kutegwa ndani ya gari uliotokea Jumamosi iliyopita
katika lango la kuingilia soko la mji mkuu wa Somalia,
Mogadishu uliua zaidi ya raia 10 wengi wao wakiwa wanawake. Hadi sasa
hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na hujuma hiyo, ingawa kundi
la kigaidi na kitakfiri la ash-Shabab limehusishwa na jinai hiyo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269