Wahajiri 550, aghalabu kutoka Afrika
Magharibi, wameokolewa kutoka katika boti zao zilizokuwa zinaelekea
kuzama katika Bahari ya Mediterranea Jumatatu katika oparesheni tano
ambapo waokoaji walipata miili mitano.
Gadi ya Pwani ya Italia iliyotekeleza oparesheni hiyo inasema
wahamiaji hao haramu walikuwa wakisafiria katika boti ndogo za
plastiki wakati waokoaji walipowaona wakizama.
Kati ya walionusuriwa ni mvulana ambaye alikuwa amezimia kwa masaa
mawili na mwanamke ambaye alikuwa amekunywa mafuta ya petroli kimakosa.
Shirika la Kimataifa la Uhamiaji IOM linasema hadi sasa wahajiri
159,496 wamefika katika pwani ya Italia kwa boti ambapo 4,271 wengine
wamepoteza maisha wakijaribu kuingia Ulaya kwa njia hiyo ya Bahari ya
Mediterranean.
Njia hatari zaidi inayotumiwa na wahamiaji haramu kuingia Ulaya
kupitia Bahari ya Mediterenea ni ile ya Libya kuelekea Italia ambapo
wasafirishaji binadamu wanatumia fursa ya kukosekana usalama katika nchi
hiyo kuwapakia watu katika boti zisizoweza kutumika baharini.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269