NA RIPOTA MAGRETH MAGOSSO MKOANI KIGOMA
ZAIDI ya wahitimu 50 kutoka Chuo
Cha Hali ya Hewa kilichopo wilaya ya kigoma
Mkoa wa Kigoma,wameaswa wafanye kazi kwa
kuzingatia weledi,maadili na taratibu za watumishi wa umma,ili kutoa huduma bora kwa maendeleo ya Taifa.
Hayo yalibainika jana kigoma
ujiji,kwenye mahafali ya 14 ya utoaji wav
yeti kwa wahitimu 33 wa ngazi ya cheti na mahafali ya tano kwa wahitimu 24 ngazi ya Stashahada waliohitimu elimu ya Anga ambapo
ikitumika sahihi taifa litajihami na majanga mbalimbali hasa
mabadiliko ya tabia nchi.
Akifafanua hilo kwa niaba ya
Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Laurent Shauri alisema wahitimu hao wamepewa mafunzo
stahiki ya watumishi wa umma ambayo
yanalenga maadili,weledi,taratibu na miongozo ya kazi ili,kuongeza ufanisi wa
kazi kwa maendeleo ya taifa na waepuke ngono
zembe inayopelekea janga la ugonjwa wa upungufu wa kinga
mwilini(UKIMWI).
Pia, chuo kinakabiliwa na
changamoto ya ukosefu wa bweni za wanafunzi na miundombinu bora ya utoaji wa
elimu hiyo ambayo ni muhimu katika kukabilina na mabadiliko ya tabia nchi na
kutoa fursa kwa wakulima kutumia utabiri huo ili kulima kilimo chenye tija
utakaonufaisha sektan hiyo.
Akifunga sherehe hizo Mgeni rasmi
ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa Emanuel
Maganga alisema taaluma yao ni chachu ya
kukabilina na mabadiliko ya tabia nchi,magonjwa na kuinua sekta ya kilimo na
kuisihi mamlaka ya hali ya hewa iongeze vifaa vya kisasa ili kutabiri ukweli itakuwa na thamani kwa jamii endapo
utabiri utakuwa wa kweli.
Mmoja wa wahitimu hao Praseda Rafaeli alisema atafanya kazi kwa uaminifu mkubwa kwa mujibu
wa miongozo ya taaluma yao ambayo ni
tija kwa taifa kukabiliana na mafuriko,ukame ambapo utabiri wa kweli ni pamoja
na vifaa vya kisasa ambavyo vitawapa mwelekeo na dira ya hali halisi ya hewa na
namna ya kukabiliana na matukio yajayo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269