Breaking News

Your Ad Spot

Dec 2, 2016

GLOBAL RESEARCH YATOA ORODHA YA WAIUNGAJI MKONO WA KIMATAIFA WA DAESH (ISIS)

Kituo cha habari cha Magharibi cha Global Reserach kimefichua katika ripoti yake mpya majina ya waungaji mkono wa kimataifa wa makundi ya kigaidi.
Global Reserach imeeleza kupitia taarifa yake kuwa nchi sita ikiwemo Saudi Arabia, Uturuki, Qatar, Uingereza, Ufaransa na Marekani pamoja na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel  ndio waungaji mkono wakuu wa makundi ya kigaidi duniani likiwemo la Daesh.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mwaka 2006 Saudia ilipokea agizo la moja kwa moja la Marekani kuitaka iunde kundi la kigaidi la Daesh nchini Iraq ili kuzuia nchi hiyo isiwe na uhusiano wa karibu na Iran. 
Rais Barack Obama wa Marekani (kulia) na Mfalme Salman bin Abdulaziz wa Saudia
Mnamo mwaka 2011 Saudi Arabia ilitoa msukumo kwa harakati za utumiaji silaha katika mji wa Dar'a kusini mwa Syria na kuyasaidia kwa fedha na silaha makundi yote ya wabeba silaha nchini humo.
Kwa mujibu wa ripoti ya Global Reserach Uturuki nayo imekuwa ikitumika kama kivuko salama kwa makundi ya wabeba silaha yanayoelekea kaskazini mwa Syria; na kwa kushirikiana na Saudia imeunda kundi la kigaidi la Jabhatu-Nusrah (Fat-hu Sham). Vilevile katika miaka ya karibuni, serikali ya Ankara imefungua mipaka ya nchi hiyo kwa ajili ya makundi ya kigaidi yanayoelekea nchini Syria.
Global Research imeendelea kufichua kupitia ripoti yake kuwa mwaka 2013, Qatar ilisaidia na kuunga mkono uundaji wa genge la kigaidi liitwalo Jaishul-Fat-h uliosimamiwa kwa pamoja na Saudi Arabia na Uturuki.
Uingereza nayo iliyasaidia kwa silaha makundi ya wabeba silaha nchini Syria kwa madhumuni ya kushirikiana kwa karibu na vikundi vidogo vidogo vya mtandao wa Al-Qaeda. Nayo serikali ya Ufaransa imekuwa ikifuata sera sawa na Uingereza katika kuyasaidia kwa silaha makundi yanayobeba silaha nchini Syria.
Wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS)
Utawala wa Kizayuni wa Israel umetajwa katika orodha ya Global Research kuwa mtoaji misaada ya zana na silaha za kivita pamoja na huduma za tiba kwa wabeba silaha wote nchini Syria. Daesh na Jabhatu-Nusrah ni miongoni mwa makundi ya kigaidi yanayopewa misaada na kuungwa mkono na utawala wa Kizayuni.
Nafasi ya Marekani katika kuliunga mkono kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh imetajwa na Global Reserach kuwa kubwa na pana zaidi kwa kusaidia harakati zote za kundi hilo katika eneo la Mashariki ya Kati.../

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages