Benjamin Sawe-MAELEZO
Rai
imetolewa kwa watumishi wa Umma kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia
sheria na taratibu ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya
kuwahudumia wananchi ili kukabiliana na umasikini.
Akizungumza
na Maelezo, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva amesema miaka
michache baada ya uhuru kumekuwa na malalamiko mengi ya wananchi dhidi
ya baadhi ya viongozi wa Umma kuhusu huduma zisizoridhisha,ubadhirifu wa
mali za umma,matumizi mabaya ya madaraka ,wizi na ukiukwaji wa haki za
binadamu
Amesema
kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, kumeleta mabadiliko
kwa watendaji wa umma katika ngazi mbalimbali za kimamlaka ukitofautisha
na miaka ya nyuma ambapo baadhi ya watendaji walikuwa wakifanya kazi
kwa mazoea.
“Viongozi
wengi wa umma walikuwa wakifanya kazi bila kujali wajibu wao na wala
hakukuwa na uwajibikaji badala ya kuwatumikia wananchi wakawa
wanatumikia matumbo yao.”Alisema Bw. Lyaniva
Alisema
Rais Magufuli ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa
wananchi ya kuwaondoa madarakani viongozi wazembe, wasiowajibika na
wasiokuwa na uwezo wa kufanya kazi katika kuwatumia wananchi.
Aliongeza
kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inastahili pongezi kwa hatua
inazochukua katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa na ufisadi
ikiwemo uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi nchini, kwani hakuna
maendeleo yatakayoweza kupatikana katika nchi pasipo na kupiga vita
rushwa.
“Ni
wajibu wa kila mwananchi kuichukia rushwa kwa vitendo ikiwemo kuwafichua
hadharani kikundi cha watu kinachojihusisha na rushwa kwani kwa kufanya
hivyo kutasaidia Tanzania kupiga hatua kubwa za maendeleo.” Alisema Bw.
Lyaniva.
Bw.
Bright Kalamba (68) mkazi wa Ubungo Msewe amesema mara baada ya uhuru
watumishi wa umma walikuwa na maadili katika utendaji wa kazi hali
ambayo ilileta matumaini kwa wananchi walioichagua Serikali iliyopo
madarakani.
Alisema
licha ya changamoto mbalimbali za baadhi ya watumishi wa umma kutokuwa
na maadili katika awamu zilizopita, ameipongeza Serikali ya awamu ya
Tano kwa kuwa mstari wa mbele kusimamia maadili ya watumishi wa umma
katika kuwahudumia wananchi.(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269