Breaking News

Your Ad Spot

Mar 17, 2017

MAREHEMU SIR. GEORGE KAHAMA AAGWA NA KUZIKWA JIJINI DAR ES SALAAM.

Rais wa awamu ya pili Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Alhaji Ally Hassan Mwinyi akitoa salamu za pole katika tukio la kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tukio hilo limefanyika jana katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, tukio hilo limefanyika jana katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Rais wa awamu ya pili Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Alhaji Ally Hassan Mwinyi akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki katika Hospitali ya Taifa Muhimbili , tukio hilo limefanyika jana katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Makamu wa Rais mstaafu Serikali ya awamu ya Nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mohammed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama alifariki  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili , tukio hilo limefanyika jana katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Mjane wa Marehemu Sir. George Clement Kahama Mama Janet Kahama  (wa pili kushoto) akiwa na familia yake wakati wa Tukio la kumuaga mume wake ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali aliyefariki katika Hospitali ya Taifa Muhimbili , tukio hilo limefanyika  katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam jana.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akitoa salamu za pole kutoka Serikalini katika tukio la kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tukio hilo limefanyika jana katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdurahaman Kinana akitoa salamu za rambirambi za Chama wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania na Chama Cha Mapinduzi katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, tukio hilo limefanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Jaji Mstaafu Mhe.Joseph Sinde Warioba akitoa salamu za pole wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, tukio hilo limefanyika  katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam jana .
Na Shamimu Nyaki-WHUSM.

Serikali imesema itaendelea kuenzi na kuheshimu mchango mkubwa katika kupigania maendeleo na ustawi wa jamii uliofanywa na marehemu Sir George Kahama enzi za uhai wake alipokuwa kiongozi katika nyadhifa mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nnauye alipokuwa akitoa salamu za Serikali katika tukio la kumuaga mmoja wa waasisi wa Taifa na Waziri msataafu marehemu Sir Gorge Kahama aliyefariki dunia Machi 12 mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Waziri Nape amesema kuwa Sir George Kahama alikuwa kiongozi mahiri na aliyetekeleza majukumu yake kwa ufasaha ambapo alikuwa miongoni mwa viongozi walioanzisha harakati za Serikali za uendelezaji wa mji wa Dodoma ikiwa ni sehemu ya kuimarisha makao makuu ya nchi.

“Marehemu Sir George Kahama tutamuenzi kwa kuendeleza yale mazuri aliyoyafanya katika kuijenga nchi yetu hasa katika ustawi wa jamii na kuimarisha uchumi wa nchi”.Alisema Waziri Nape.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdurahaman Kinana amumueleza Sir George Kahama kama kiongozi mahiri katika Chama aliyependa maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla katika weledi wa hali ya juu na alikuwa mchapakazi.

“Sir George Kahama alikuwa mtumishi na kiongozi aliyetukuka ametuachia hamasa kubwa ya kuwa viongozi bora zaidi na wenye mapenzi na Taifa letu katika kuleta maendeleo.”Alisema Ndugu Kinana.

Marehemu Sir George Kahama amekuwa Waziri na Kiongozi kabla na Baada ya Uhuru wa Tanzania Bara kuanzia awamu ya kwanza hadi ya tatu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo amezikwa  Jijini Dar es Salaam jana na ameacha Mjane na Watoto.

1 comment:

  1. Salaam nyingi za rambi-rambi kwa familia ya Sir George Kahama. May Sir George Kahama Rest in Peace.

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages