Rais wa
Zanzibar na Mwenyekikti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto)
alipokuwa akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya, Mkoa wa Kusini
Pemba Mhe, Hemed Suleiman (kushoto kwake) alitembelea Kijiji cha Makombeni kuangalia
nyumba mbali mbali za Wananchi zilizopatwa na athari zilizotokana
na Mvua zinazoendelea kunyesha kisiwani humo jana Mei 15, 2017 wakati alipofanya
ziara maalum ya kikazi.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekikti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
(kushoto) alipofika kijiji cha Gando kumfariji na kumpa pole Mzee Juma Mjaka
Khamis (kulia) akiwa na Familia yake aliyepata maafa ya nyumba yake kuangukiwa
na mti na kupelekea kukosa sehemu ya kuishi baada ya mvua kubwa za masika
zilizonyesha hivi karibuni kisiwani humo
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekikti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (wa pili
kushoto) alipokuwa akiangalia jengo la ZSTC Mkoani Pemba ambalo ukuta wake
umeanguka kutokana na kuangukiwa na mti baada ya mvua kubwa za masika
zilizonyesha hivi karibuni na kusababisha uharibifu mkubwa alipofanya ziara
maalum kisiwani humo Mei 15, 2017. (PICHA NA IKULU ZANZIBAR)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269