Breaking News

Your Ad Spot

May 18, 2017

KINANA AONGOZA KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA VYAMA RAFIKI NCHINI ANGOLA

Na Bashir Nkoromo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ameongoza majadiliano na viongozi wa vyama rafiki kikiwemo Chama Cha Kikomunisti cha China, vilivyoshiriki Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika.

Katika Mkutano Kinana amefuatana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole, Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga na Watendaji kutoka Jumuia za Chama Cha Mapinduzi.

Taarifa kutoka Angola, zimesema, katika Mazungumzo hay, vyama rafiki vimepongeza mabadiliko yalivyofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hiv karibuni ambayo yamepewa jina la CCM MPYA, TANZANIA MPYA.

Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika ni pamoja na MPLA cha Angola, ANC cha Afrika Kusini, ZANU-PF cha Zimbabwe,  MPLA cha Angola, FRELIMO cha Msubiji, SWAPO cha Namibia na TANU ambacho sasa ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages