Muhitimu wa elimu ya juu, akisoma kipeperushi chenye maelezo ya shughuli
zifanywazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wakati wa mahafali ya pili ya
kitaifa ya wahitimu wa elimu ya juu waliofanya vizuri kwenye vitivo vyao
mwaka 2016.Mahafali hayo yaliyowaleta pamoja zaidi ya wahitimu 100
yalidhaminiwa na Mfuko huo na kufanyika makao makuu ya PSPF jijini Dar
es Salaam Mei 19, 2017
Baadhi ya wahitimu hao wakiimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa mahafali
Bw. Chacha Nyaikwabe, Meneja Kumbukumbu
wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu
udhamini wa PSPF kwenye mahafali hayo. Bw. Chacha alisema, PSPF imeamua
kudhamini mahafali hayo kwa vile inajua fika, wahitimu hao ni watu
muhimu wa kujiunga na Mfuko huo na kwa hali hiyo Mfuko umepata fursa ya
kuwaeleza shughuli mbalimbali zifanywazo na PSPF ikiwa ni pamoja na
kusajili wanachama na Mafao yatolewayo na Mfuko huo kwa Mwanachama.
Rais wa TAHILISO, akizungumza kwenye mahafali hayo. Mahafali hayo yameratibiwa na TAHILISO. Kulia ni mgeni rasmi,
Margareth Komba, Naibu Mkurugenzi Elimu ya Juu Sayansi na
Ubunifu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, na kushoto ni mwakilishi kutoka PSPF, Bw.Nyaikwabe.
Mgeni rasmi Bi. Margareth Komba, Naibu Mkurugenzi Elimu ya Juu Sayansi na
Ubunifu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, akizungumza wakati wa mahafali hayo
Wahitimu wakifurahia hotuba
Wahitimu wakisikilzia kwa makini kilichokuwa kikiendelea
Muhitimu akisoma kipeperushi chenye maelezo ya shughuli zifanywazo na PSPF
Wahitimu wakiwa kwenye matembezi ya mahafali ya kitaifa ya pili ya wahitimu wa elimu ya juu chini Tanzania.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269