Sehemu ya wajumbe waliohudhuria
Mkutano Mkuu wa Chama Cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) ambapo mgeni
rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Samia Suluhu Hassan. (PICHA ZOTE NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
Makatibu Muhtasi wakifurahia hotuba ya Mama Samia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza Makatibu Mahsusi
nchini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na waache tabia ya kutoa
siri za ofisi zao kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.
NA
MWANDISHI MAALUM
MAKAMU
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza
Makatibu Mahsusi nchini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na waache tabia ya
kutoa siri za ofisi zao kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli
hiyo wakati anafungua mkutano wa Tano wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania
katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Mjini Dodoma.
Makamu
wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema uadilifu na uaminifu ni njia pekee ya
kuaminiwa na viongozi wao hivyo ni muhimu kwa makatibu mahsusi nchini kufanya
kazi kwa bidii na ubunifu mkubwa katika maeneo yao ya kazi.
Makamu
wa Rais pia amewahimiza makatibu mahsusi kufanya tathmini ya utendaji wao wa
kazi na wawe tayari katika kujifunza mbinu mpya za utendaji zinazoendana na
mabadiliko ya teknolojia.
“Sote
tunafahamu kuwa dunia imekuwa ni kijiji kutokana na utandawazi unaoletwa na
mifumo ya teknolojia hivyo kutokana na mabadiliko haya hamna budi nanyi
kubadilika na kwenda na wakati ili msiangaliwe kwa mtazamo hasi wa kuwa wapiga
cha tu”
Kuhusu
uanzishwaji wa Shahada ya Uhazili, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan
amewahakikishia makatibu mahsusi kuwa Serikali imekubali kuanzisha shahada hiyo
ambapo masomo yake yataanza mwezi wa Tisa mwaka huu kwenye Chuo cha Utumishi wa
Umma Tanzania katika mikoa ya Dar es Salaam na Tabora.
Makamu
wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahimiza makatibu mahsusi kuchangamkia fursa
hiyo kwa ajili ya kujiendeleza kielimu kwa kuzingatia kuwa elimu haina mwisho.
Kwa
upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Angellah Kairuki amesema Serikali inafanyia kazi baadhi ya kero
zinazowakabili makatibu mahsusi ikiwemo kuboresha maslahi ya kada ya uhazili
nchini.
Amesema
lengo la Serikali ni kuhakikisha kada hiyo pamoja na watumishi wengine wanapata
maslahi bora ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza ufanisi kazi.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269