Breaking News

Your Ad Spot

Jul 15, 2017

MKURUGENZI KAYOMBO AKUSANYA MILIONI 150 KWA MWEZI KATIKA SOKO LA NDIZI-MABIBO ILIHALI AWALI ZILIKUSANYWA MILIONI 10 KWA MWEZI

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akizungumza na wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakati wa ziara ya kikazi katika eneo hilo.
Wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakifatilia kwa makini mkutano
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John lipesi Kayombo akitafakari kwa makini changamoto mbalimbali za wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakati wa ziara ya kikazi katika eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori (Kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakati wa ziara ya kikazi katika soko la Ndizi-Mabibo
Wakuu wa Idara na Vitengo Manispaa ya Ubungo wakifatilia mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori uliofanyika katika Soko la Ndizi-Mabibo Jijini Dra es salaam
Wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakifurahi mara baada ya kuambiwa wataendelea na shughuli zao katika soko hilo.

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo amebaini ubadhirifu wa kiasi kikubwa cha pesa zinazofikia shilingi milioni tisini kila mwezi, unaofanywa na kikundi kinachojiita Majimoto kinachodai kupewa jukumu la kukusanya mapato katika soko la matunda la Mabibo kwa niaba ya mmiliki wa eneo hilo ambaye ni Kiwanda cha Nguo cha Urafiki.

Mkurugenzi Kayombo amesema kuwa ubadhirifu huo umebainika baada ya Halmashauri ya Manispaa kuchukua jukumu la kusimamia kwa muda ukusanyaji mapato katika soko hilo ambapo makusanyo yamepanda kutoka shilingi milioni saba zilizokuwa zinakusanywa hapo awali hadi zaidi ya shilingi milioni mia moja.

Kayombo amesema hayo wakati wa ziara ya ghafla iliyofanyika sokoni hapo na kuongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori kwa ushirikiano wa pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo sambamba na watendaji wote katika Manispaa hiyo,

Ziara hiyo imejili mara baada ya uongozi wa kiwanda cha Urafiki kutaka kuwaondoa kwa nguvu wafanyabiashara na kulifunga eneo hilo kwa kujenga uzio utakaozuia ufanyaji wa biashara.

Mkurugenzi amejibu hapo hapo agizo la Mkuu wa Wilaya Mhe Makori lilomtaka kusitisha mara moja zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara hao kwa kuwaagiza Afisa Afya na Mazingira wa Manispaa ya Ubungo kufuatilia malalamiko yaliyotolewa na wananchi katika mkutano huo kuhusu kiwanda cha nguo cha Urafiki ambacho kinalalamikiwa na wananchi kwa kuathiri afya zao kutokana na Moshi unaotoka kiwandani hapo.

Aidha mbele ya umati wa wafanyabiashara na wananchi katika mkutano huo Mkurugenzi Kayombo amemuagiza Kaimu Injinia wa Manispaa ya Ubungo kusambaza kifusi cha mawe kilichomwagwa sokono hapo kwa ajili ya kuzuia mlundikano wa maji.

Mkurugenzi Kayombo alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli imedhamiria kukusanya mapato kwa kiasi kikubwa hivyo ameeleza dhamira yake ya kukusanya mapato ya Zaidi ya shilingi milioni 150 kwa mwezi katika soko la Ndizi-Mabibo na tayari mirija na mianya yote ya rushwa amefanikiwa kuiziba kwa kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages