Breaking News

Your Ad Spot

Jul 2, 2017

RAIS DK. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UBORESHAJI BANDARI YA DAR ES SALAAM

 Rais Dk. John Magufuli akiwa na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird wakizindua jiwe la msingi la mradi wa Uboreshaji Bandari ya Dar es Salaam, katika hafla iliyofanyika leo eneo la Bandari hiyo. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa
 Jiwe la Msingi
 Rais Dk. John Magufuli akimshukuru Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird  baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Uboreshaji Bandari ya Dar es Salaam
 Rais Dk. John Magufuli akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
 Baadhi ya waalikwa wakiwemo mabalozi kutoka nchi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Rais Dk. John Magufuli aliyoioa kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam
 Rais Magufuli akimpongezwa na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird, baada ya kutoa hotuba yake kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam 
 Rais Dk. John Magufuli akionyeshwa jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird wakati wakitazama kipeperushi cha maelezo ya Mradi wa uboreshaji wa Bandari jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla hiyo.
 Rais Dk. John Magufuli na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird wakifurahia jambo  wakati wa hafla hiyo
 Rais Dk. John Magufuli akishiriki kuimba wimbo wa taifa akiwa na viongozi mbalimbali wakwemo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird, baada ya kuwasili katika eneo la Bandari jijini Dar es Salaam,kuanza hafla hiyo
 ais Dk. John Magufuli akipiga makofi pamoja na viongozi wengine waliosimama wakati Mjomba Band walipokuwa wakiimba wimbo wa 'Aamka Tufanye kazi' kabla ya tukio la uwekaji wa jiwe la msingi Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
 Rais Dk. John Magufuli akishiriki kucheza muziki wakati Mjomba Band ilipokuwa ikitumbuiza  baada ya uwekaji wa jiwe la msingi Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam. Kushoto ni mwanamuziki wa bendi hiyo Banana Zorro na Wapili kulia ni Kiongozi wa Bendi hiyo Mrisho Mpoto
Rais Dk. John Magufuli akicharza tumba, wakati Mjomba Band ilipokuwa ikitumbiza baada ya tukio la uwekaji wa jiwe la msingi Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam. Imetayarishwa na Bashir Nkoromo. PICHA: IKULU

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages