Breaking News

Your Ad Spot

Sep 19, 2017

BULEMBO ATANGAZA KUNG'ATUKA KUGOMBEA UENYEKITI JUMUIA YA WAZAZI, LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na waandishi wa habari leo, Makao Makuu ya Jumuia hiyo jijini Dar es Salaam, kutangaza uamuazi wake wa kutogombea katika Jumuia hiyo.
-----------------------------------
NA BASHIR NKOROMO
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania, Alhaji Abdallah Bulembo mchana huu ametangaza kujiondoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Jumuia hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa ndani ya Chama unaofanyika mwaka huu.

Bulembo ambaye alikuwa ameshachukua fomu kuwania Uenyekiti wa Jumuia ya Wazazi, Taifa, kwa awamu ya pili ametangaza uamuzi huo, mbele ya waandishi wa habari aliowaita Ofisini kwake Makamo Makuu ya Jumuia hiyo jijini Dar es Salaam.

"Mwanzoni kabisa nilitangaza kutogombea, lakini kwa shinikizo la wazee maarufu ndani ya Chama akiwemo Mzee Malecela (John Malecela), na wengineo niliamua kuchukua fomu, lakini sasa leo bila kuomba ushauri kwa yeyote nimeamua kutangaza kuwa sigombei tena".

"Uamuzi huu nimeufikia baada ya kuona kwamba katika kinyang'anyiro hiki kwenye nafasi ya Uenyekiti tulijitokeza wagombea 49. Sasa nina uhakika baada ya kujitoa mimi katika 48 waliobaki lazima atapatikana Mwana CCM ambaye viatu vyangu vitamtosha", alisema Bulembo.

Amesema ameamua kujitoa kugombea siyo kwa shinikizo lolote kwa kuwa kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi ndani ya Chama hakuna sehemu yoyote inayomzuia kuwania uongozi.

Builembon amesema, anafurahi kwamba Jumuia ya Wazazi anaiacha ikiwa bora kuliko alivyoikuta, akisema, hivi sasa hadhi ya shule za jumuia hiyo imepanda kitaaluma, na pia Jumuia imeweza kulipa asilimia 68 ya madeni aliyokuta ikidaiwa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages