Breaking News

Your Ad Spot

Oct 30, 2017

RAIS DK MAGUFULI AENDA MWANZA LEO

Rais Dk. John Magufuli akiagana na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam kwenda mkoani Mwanza leo.


DAR ES SALAAM
Rais Dk. John Magufuli, leo Jumatatu, Oktoba 30, 2017, ameondoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Mwanza, ambapo akiwa mkoani humo pamoja na mambo mengine atafungua mradi wa ujenzi wa daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu, imesema pia Rais Magufuli atafungua kiwanda cha iinywaji baridi cha Sayona kilichopo Nyakato mkoani humo na baadaye kufanya mkutano wa hadhara.

Katika Uwanja wa Ndege wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Rais Magufuli ameagwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages