Breaking News

Your Ad Spot

Nov 17, 2017

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE YA NYABANGE NA KITUO CHA KULELEA WATOTO CHA JIPE MOYO MKOANI MARA

Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akiongea na Wazee katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara wakati wa Tume ilipotembelea makazi hayo ikiwa ni sehemu ya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
Sehemu ya wazee katika Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara wakimsikiliza katibu Msaidzi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa. 
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akimkabidhi zawadi ya Sabuni Mkuu wa Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nyabange iliyopo Butiama mkoani Mara Bw. Edward Mbaga wakati Tume ikifanya Utafiti mkoani humo. Kushoto ni Mhadhiri Msaidizi Chuo cha Ustawi wa Jamii Bw. Paulo Mwangosi
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akiongea na Wazee wa Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara wakati wa Tume ilipotembelea makazi hayo ikiwa ni sehemu ya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
Sehemu ya Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara.
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bi. Agnes Mgeyekwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na uongozi wa kituo cha kulelea watoto cha Jipe Moyo kilichopo Musoma mkoani Mara. Katikati ni mratibu wa kituo hicho sister Annunciata Chacha
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akimkabidhi zawadi ya Sabuni na Juisi Mratibu wa Kituo cha Kulelea Watoto cha Jipe Moyo Sister Annunciata Chacha wakati Tume ikifanya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Bi Agnes Mgeyekwa (wa tatu kushoto) na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika Kituo cha Jipe Moyo kilichopo Musoma mkoani Mara wakati Tume ikiendesha Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania. Kushoto ni Mratibu wa Kituo hicho Sister Annunciata Chacha.
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bi Agnes Mgeyekwa akisalimiana na mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha Jipe Moyo kilichopo Musoma mkoani Mara wakati Tume ikifanya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages