Breaking News

Your Ad Spot

Dec 16, 2017

KUWAIT YALAANI MAUAJI YA WANAJESHI WA TANZANIA HUKO DRC

 Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem (wakwanza kushoto) ameungana na mamia ya viongozi wa Serikali akiwemo Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali katika uwanja wa ndege wa Zanzibar, ameungana nao kupokea na kuaga miili ya wanajeshi wa Tanzania waliopoteza maisha yao huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakilinda amani chini ya muavuli wa umoja wa mataifa. Al- Najem amesema kuwa Serikali ya Kuwait inalaani vikali tukio la kushambuliwa wanajeshi wa Tanzania na kupelekea wanajeshi 14 kufariki huku wengine 44 wakijeruhiwa. Ameongeza kuwa' tumefuatulia tukio hili la kushambuliwa wanajeshi wa kulinda amani katika kambi yao huko Kongo kwa huzuni kubwa, ambapo Serikali ya Kuwait inakemea
vikali mashambulizi yanayolenga vikosi vya kulinda amani au mashirika ya kibinadamu'. hayo ameyasema
wakati wa ziara yake ya kikazi visiwani Zanzibar, Balozi Al-Najem amuomba Mwenyezi Mungu awarehemu wanajeshi waliouwa na kuwaponesha kwa haraka waliojeruhiwa

Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi (wa pili kushoto) aongoza mamia kupokea na kuaga miili ya wanajeshi wa Tanzania waliopoteza maisha yao huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakilinda amani chini ya muavuli wa umoja wa mataifa katika uwanja wa ndege wa Zanzibar,

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages