Breaking News

Your Ad Spot

Dec 18, 2017

MKUTANO MKUU WA CCM WARINDIMA DODOMA, LEO DK. MAGUFULI AMTAKA TENA KINANA, WAJUMBEA WASHANGILIA KUUNGA MKONO

 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli akifungua Mkutano Mkuu wa tisa wa CCM, katika Ukumbu wa Jakaya Kikwete, Dodoma, leo. Pamoja na mambo mengine kuhusu mageuzi ndani ya Chama, uadilifu na usimamizi wa mali za Chama ili Chama kisitegemee wafadhili wakiwemo matajiri wachache, amemtaka Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Kkatibu Mkuu katika kipindi kingine cha miaka mitano
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimsalimia Balozi wa China hapa nchini Wang Ke, alipokuwa akisalimia mabalozi kutoka nchi mbalimbali ambao wamehudhuria Mkutano huo 
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo wakikagua mazingira ya nje ya ukumbi kabla ya mkutano huo mkuu kuanza
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akiandaa mazingira ya kuchangamsha ukumbi kabla ya mkutano huo kuanza. Kushoto ni katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
 Wanakwaya wa TOT wakiimba wimbo maalum wa kumkaribisha ukumbini Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli
 Wajumbe wakijimwayamwaya ukumbini kushangilia wakati Mwenyekiti wa CCM Taifa, akiingia ukumbini
 Mwimbaji wa TOT akiimba wimbo wa kuhamasisha mapokezi ya Mwenyekiti ukumbini
 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Jakaya Kikwete na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ali Hassan Mwinyi wakimsubiri Mwenyekiti Kuingia Ukumbini. Mzee Mwinyi akisoma toleo maalum la gazeti la Uhuru wakati akisubiri
 Viongozi waliotangulia meza kuu wakisimama kumlaki Mwenyekiti wa CCM rais Dk John Magufuli wakati akiingia ukumbini
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akisalimia viongozi mbalimbali baada ya kuingia ukumbini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akiwa tayari ukumbini. Wengine kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mstaafu Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa Zanzibar Dk. Shein, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM-bara Philip Mangula na Mwenyekiti Mstaaafu wa CCM Benjamin Mkapa
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Maguduli akijadili jambo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana baada ya kuketi ukumbini
 Waimbaji wa TOT wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya Mkutano kuanza
 Wajumbe wakiwa wamesimama kuimba wimo wa Taifa
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli na viongozi wengine meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa huku wamesimama kwa ukakamavu 
 Viongozi wakiw wameketi baada ya kuimba wimbo wa taifa
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiondoka meza kuu kwa ukakamavu kwenda kufuatilia jambo
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti kufungua Mkutano huo
 Wapicha picha wakifuatilia matukio
 Mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Mama Maria Nyerere akiwa na Mama Salma Kikwete kwenye mkutano huo
 Baadhi ya wageni waalikwa na wajumbea wakiwa kwenye mkutano huo
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli (kulia)akifungua mkutano huo mkuu
 Wajumbe wakishangilia baada ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kumtaka Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Ukatibu Mkuu kwa miaka mingine mitano
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akionekana kutafakari baada ya kauli ya Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli  kumhitaji tena
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiinuka kuonyesha ishara ya kukubali makakwa ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Magufuli. Kulia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Zanzibar Dk Amani Abeid Karume na Mzee Mkapa ambaye anacheka kuonyesha kuunga mkono
 Baadhi ya waliohamia CCM kutoka vyama vya upinzani wakisimama baada ya kutmbulishwa na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kwenye mkutano huo
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli akipongezwa na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Jakaya Kikwete baada ya hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Bara Pius Msekwa 
 "Hotuba imeshiba" inaelekea ndivyo Kikwete alivyomwambia Dk Magufuli baada ya kumpongeza 
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimpongeza Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli baada ya hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo
 Dk Magufuli akipongezwa na Makamu Mweenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula kwa hotuba nzuri ya ufunguzi wa mkutano huo
 Dk. Magufuli akipongezwa na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Zanzibar Amani Karume baada ya hotuba
 Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli akirudi katika nafasi yake baada ya kutoa hotuba na kufungua mkutano huo
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akitoa maelezo kuhusu CCM ilivyotekeleza kazi zake katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. kabla ya hapo alitumia fursa hiyo kumshukuru Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli kwa kumwamini tena ili aendelee kumsaidia. Kinana amemwahidi kumsaidia kwa weledi na uaminifu mkubwa
TOT wakimshangilia Mwenyekiti Dk. Magufuli baada ya hotuba yake

KABLA YA MKUTANO

 Kabla ya mkutano kuanza, baadhi ya wajumbe wakiperuzi nakala za toleo maalum la gazeti la Uhuru kuhusu mkutano huo
 Wajumbe wakipozi picha ya kumbukumbi ukumbini
 Baadhi ya wafanyakazi waandamizi wa Uhuru Publications Ltd, wachapichaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani wakiwa ukumbini
 Mwanadiplomasia akisoma gazeti la Uhuru
 Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM Bara John Chiligati akisoma toleo maalum la gazeti la Uhuru
 Katibu Mwenezi wa CCM Humphrey Polepole akijadili jambo na Afisa Mwandamizi wa CCM Frank Uhahula. kulia ni Kanali Mstaafu Ngemela
 Maofisa wa CCM wakiwa ukumbini kusimamia masuala ya Itifaki
 Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Yusuf Makamba akisalimiana na Mzee John Butiku
 Vijana Jazz wakirindima ukumbini
 Baadhi ya watangazaji wa UHURU FM wakiwa nje ya ukumbi kurusha live matangazo ya mkutano huo mkuu
 Baadhi ya wageni waalikwa wakisalimiana ukumbini
 Mama Janet Magufuli akiwasili ukumbini


 Wajumbe ukumbini
 Wajumbe ukumbini
 Wapigapicha Muhidin Issa Michuzi aka Ankal na Adam Mzee wakicheki mazingira ukumbini
 Wafanyakazi wa Makao Makuu ya CCM, Lumumba wakiwa ukumbini
 Wasanii wa TOT wakipumzika ukumbini baada ya awamu ya kwanza ya kutumbuiza kumalizika PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages