Breaking News

Your Ad Spot

Mar 11, 2018

WAZIRI MWAKYEMBE AZINDUA KITUO CHA RADIO JAMII CHA TBC JIJINI ARUSHA

 Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio Jamii cha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) chenya masafa ya 92.1  leo Jijini Arusha
 Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe akiangalia mitambo ya kurusha matangazo katika studio za kituo kipya cha redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha mara baada ya kukizindu rasmi
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza katika hafla ya kuzindua kituo cha Redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Mjumbe wa Bodi ya TBC Dk. Hassan Abbas, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Gabriel Daqqaro na kushoto ni Mkurugezni wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi. Peter Ulanga na wa pili ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dk. Ayoub Rioba
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza Fundi Mitambo wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC)  Lucy Mgala alipotembelea mitambo ya TBC iliyoko Njiro Jijini Arusha
 Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) alipata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kanda ya Arusha wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Gerald Uisso (kushoto) na kulia ni Fundi Mitambo TBC Lucy Mgala
 Wananchi wa Arusha wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, alipokuwa akihutubia katika halfa ya uzinduzi wa kituo cha Redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya TBC, Uongozi wa TBC na Wakandarasi walijenga kituo cha Redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha.(Picha Na Ismail Ngayonga).

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages