Breaking News

Your Ad Spot

Apr 6, 2015

MASAUNI AKIKABIDHIWA CHETI KWA MCHANGO WAKE KWA VIJANA DHIDI YA AMANI KUTOKA UNESCO NA YUNA

Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni na Mlezi wa Jumuiya ya Tanzania Yuoth Icon (TAYI) Mhe.Eng Hamadi Yussuf Masauni akikabidhiwa Cheti cha Mchango wake kwa Vijana kuhusiana na Amani kutoka kwa Mratibu wa UNESCO kwa Vijana Tanzania Ndg Simba Mwinyi Simba kwa kutambua mchango wake kwa Vijana Zanzibar kudumisha amani, hafla hiyo mefanyika katika Kituo cha Vijana cha TAYI muembemadema Zanzibar    
Mhe.Eng Hamad Masauni akionesha Cheti baada ya kukabidhiwa wakati wa Kongamano la Vijana wa TAYI baada ya kukabidhiwa, 
Naibu Katibu wa Vijana wa Umoja wa Mataifa Tanzania(YUNA) Bi, Pili Khamis, akikabidhi Cheti kilichotolewa na YUNA kwa kuthamini Mchango wake kwa Vijana Zanzibar Mhe.Eng Hamad Yussuf Masauni, makabidhiano hayo yamefanyika katika jengo la Ofisi za TAYI muembemadema Zanzibar kushoto Mratibu wa YUNA Zanzibar Ndg Ali Hemed.   
Mhe.Eng. Masauni akioneshga Cheti chake baada ya kukabidhia kilichotolewa na YUNA kujali mchango wake kwa Vijana Zanzibar.
Vijana wa Kituo cha TAYI wakifuatilia hafla hiyo ya makambidhiano ilioendana na Kongamano la Vijana kuhusiana na Amani Zanzibar wakati wote, Kongamano hilo limetayarishwa na Unesco kwa kushirikiana na Jumuiya ya TAYI.
Mhe Eng.Hamad Yussuf Masauni, akizungumza na Vijana wakati wa hafla ya kukabidhiwa Vyeti ilioendana na Kongamano la Vijana kuhusiana na Amani Zanzibar lililowashirikisha vijana wa TAYI na wa Vyuo Vikuu Zanzibar lililofanyika katika Kituo cha TAYI Muembemadema Zanzibar na kudhaminiwa Unesco. 
Mratibu wa Unesco Tanzania kwa Vijana Ndg Simba Mwinyi Simba akizungumza wakati wa Kongamano hilo la Mafunzo ya kudumisha Amani kwa Vijana Tanzania lililofanyika katika kituo cha Vijana cha TAYI muembemadema Zanzibar na kushirikisha Vijana kutoka Vyuo Vikuu Zanzibar na Mabalozi wa Vijana wa Amani. 
Mratibu wa YUNA Ndg Ali Hemeid akizungumza na kutowa mafunzo kwa Vijana walioshiriki Kongamano hilo.
Mhe Eng. Hamad Yussuf Masauni, akiwa katika picha ya pamoja na Vionhozi wa Vijana na Mabalozi wa Amani wa Vijana Zanzibar baada ya kumalizika kwa Kongamano hilo na kumkabidhi Chrti Mhe Masauni cha kujali Ushiriki wake kwa Vijana dhidi ya Amani. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages