Breaking News

Your Ad Spot

Apr 22, 2016

RAIS IDRISS DEBY ATANGAZWA KUWA MSHINDI WA UCHAGUZI WA CHAD

Rais Idriss Déby atangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Chad
Rais Idriss Déby wa Chad ametangazwa kuwa mshindi wa uchagumzi mkuu uliofanyika hivi karibuni nchini Chad.
Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo imemtangaza rais huyo kuwa ndiye mshindi katika uchaguzi huo na hivyo kuwa rais kwa muhula wa tato mfululizo nchini Chad. Kwa mujibu wa tume hiyo, Rais Idriss Déby amepata asilimi 60 ya kura, huku mpinzani wake Saleh Kebzabo akipata asilimia 12 ya kura hizo. Tayari Kebzebo amepinga matokeo hayo akisema kuwa, kulifanyika uchakachuaji mkubwa wa kura kwa maslahi ya Rais Déby. Aidha mwanasiasa huyo amesema kuwa mbali na uchakachuaji huo, mamia ya masanduku ya kura yalipotea, na kusisitiza kuwa, raia wa Chad hawawezi kukubaliana na matokeo hayo. Wiki iliyopita waangalizi wa Umoja wa Afrika kwenye uchaguzi huo walinukuliwa wakisema kuwa, uchaguzi nchini Chad ulifanyika katika anga huru na salama. Itafahamika kuwa, Rais Déby amekuwa madarakani tangu mwaka 1990, baada ya kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo, dikteta Hissène Habré. Uchaguzi Mkuu nchini Chad ulifanyika tarehe 10 ya mwezi huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages