Meneja wa Uingereza Fabio Capello (Pichani), amelaumu pesa nyingi wanazopewa wachezaji wake kwa mizozo inayowakumba.
Capello anasema mizozo hiyo, ambayo inatishia kuathiri matumaini ya timu ya Uingereza katika kombe la dunia, imekumba wachezaji katika nchi zingine pia kama vile Italia, Ujerumani na Uhispania.
Wachezaji kadhaa wa timu ya Uingereza wamehusika katika mizozo ya kimapenzi hivi majuzi. Kapteni wa timu hiyo John Terry alitimuliwa kutoka wadhfa wake kufuatia mzozo wa kimapenzi na aliyekuwa mpenzi wa mchezaji mwenzake katika timu ya Chelsea hapo zamani, Wayne Bridge.
Bridge, ambaye hakumsalimia Terry wakati timu anayoichezea, Manchester City ilikutana na Chelsea wikendi iliyopita, amesema kwamba hataichezea timu ya Uingereza kwa sababu ya mzozo huo.
Mchezaji mwingine wa timu hiyo, Ashley Cole, pia aligonga vichwa vya habari mwezi jana baada ya kuachana na mke wake Cheryl. Timu hiyo ya Uingereza itakutana na Misri hii leo. http://www.bbcswahili.com/
Your Ad Spot
Mar 3, 2010
Home
Unlabelled
CAPELLO ALAUMU MALIPO YA WACHEZAJI
CAPELLO ALAUMU MALIPO YA WACHEZAJI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269