Breaking News

Your Ad Spot

Mar 28, 2010

MNEC-CCM AWAPA WAZAZI OFA YA PUNGUZO 40% KUSOMESHA WATOTO SHULE YAKE YA ST. ANNE MARIE

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Jason Rweikiza akifungua ofisi ya CCM tawi la Msingwa, Kata ya Mbezi Dar es Salaam, jana. Rweikiza alitoa pia mchango wa sh. 500,000 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa ofisi hiyo.Rweikiza na viuongozi wa Kata ya Mbezi wakisalimia wanachama wakati wa sherehe hiyo ambayo iliambatana na kukabidhiwa bendera ya Chama Wajumbe 15 wa CCM waliochaguliwa hivi kiaribuni na katika kata hiyo.MWENYEKITI wa CCM Kata hiyo,  Amir Majembe akimvisha mkanda maalum Rweikiza ambao alipewa kwa hehima ya wazee wa Mbezi Deo Ndunguru (wapili kulia) na Juma Nkangaa.(kulia)Rweikiza akimkabidhi bendera ya CCM Mjumbe wa shina namba 13, Mussa Geuza, mmoja kati ya wajumbe 15 wa CCM katika kata hiyo ambao aliawakabidhi bendera hizo kufuatia kuchaguliwa kwao hivi karibuni.Rweikiza akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wazee wa Kata ya Mbezi baada ya kupewa heshimakwa kupewa mkuki wa kukihami Chama.MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Jason Rweikiza akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe 15 wa CCM, baada ya kuwakabidhi bendera za Chama, katika hafla iliyofanyika jana, katika kata ya Mbezi, Dar es Salaam.
Habari Kamili
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) CCM, Jason Rweikiza ametoa punguzo aslimia 40 kwa kila mkazi wa Kata ya Msingwa, Mbezi, Dar es Salaam, atakayepeleaka mototo katika shule yake ya St. Anne Marie iliyopo eneo hilola Kimara.

     Rweikiza alitoa ‘ofa’ hizo, baada ya kufungua Ofisi ya CCM tawi la Msingwa katika hafla iliyoambatana na kuwakabidhi bendera za CCM wajumbe 15 wa mashina ya CCM waliochaguliwa katika wa kata hiyo.
    "kutokana na kwamba nimekuwa eneo hili na kufanya shughuli zangu hapa na wengi wenu hapani wana-CCM wenzangu, natoa ofa ya punguzo la asilimia 40 ya ada, kwa mzazi wa hapa atakayeleta mototo wake kwenye shule yangu ya St. Anne Marie iliyopo hapa Mbezi”, alisema Rweikiza.
     Shule hiyo ya St Anne Marie, inatoa masomo ya shule za awali, msingi, sekondari hadi kidato cha sita.
Pia aliahidi kutoa mchango wa sh. 500,000 kwa ajili yak umalizia ujenzi wa ofisi ya CCM aliyofungua, na kueleza kwamba ofa la punguzo la ada na msaada wa fedha hizo hatoi kwa sababu ya maadalizi ya kugombea ubunge kwa kuwa hana nia ya kuwania nafasi hiyo.
      Rweikiza aliwataka wanachama wa CCM kulitumia tawi hilokuzingumza mambo muhimu ya ujenzi wa Chama kwa kufanya vikaovyote vya chama kwamujibu wa Katiba.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages