Breaking News

Your Ad Spot

Mar 24, 2010

MWENYEKITI WA CCM, TAIFA, RAIS JAKAYA KIKWETE ATINGA KATIKA OFISI YAKE YA UENYEKITI WA CHAMA, OFISI NDOGO YA MAKAO MAKUU YA CCM, LUMUMBA, DSM

HABARI KATIKA PICHAHALI ilivyokuwa kwenye Ofisi Ndogo ya Makao makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam, wakati akisubiriwa Mwenyekiti wa Chama taifa, Rais jakaya Kikwete,  Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba wakati wakimsubiri Mwenyekiti wa CCM Taifa kuwasili kwenye ofisi yake ya Uenyekiti  leo.MHARIRI Mtendaji wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd ( UPL) Josiah Mufungo (wapili kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Uhuru FM, Mikidadi Mahamud (kulia) na Meneja Rasilimali Watu na Fedha wa UPL, Lucas Anthony Kisasa (wapili kushoto) na aliyekuwa Katibu Mkuu wa kilichokuwa Cha Cha Soka Tanzania (FAT), Wambura.Baadhi ya wadau wa Chama wakimsubiri kwa hamu Mwenyekiti wa Chama, Rais Kikwete.MSAIDIZI wa katibu Mkuu wa CCM, kuhusu masuala la habari, Mwilapwa akifurahia jambo na Wapigapicha wa Rais, Juma Kengele na Freddy Maro wakati wa mida ya mwishomwisho kabla ya mwenyekiti wa Chama kuwasili.Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete akilakiwa na Makamu wa CCM (Bara) Pius Msekwa alipowasiliMwenyekiti wa CCM taifa, Rais jakaya Kikwete akisalimia baadhi ya viongozi wa Chama waliomsubiri.Mwenyekiti wa Chama, Rais Jakaya Kikwete baada ya kuwasili katika ofisi yake ya Uenyekiti wa CCM, katika Ofisi Ndogo ya Makao makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) George Mkuchika,  Makamu Mwenyekiti (Bara) Pius Msekwa na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Yussuf Makamba .JK akitia saini kitabu katika ofisi yake ya Uenyekiti wa CCM taifa. KATIBU Mkuu wa UVCCM,  Martine Shigella akisalimiana na Ofisa wa Makao Makuu ya UWT, Sarah Msafiri wakati JK akiwa ofisini kwake. Kati yao ni Mkuu wa vipindi wa UHURU FM, Anjel AkilimaliKATIBU Mkuu wa UVCCM Martine Shigella akipena namba za simu na Edward M. au 'Edo' ambaye ni msaidizi wa Katibu Mkuu wa CCM Yussuf Makamba. Kwa sasa Edo anauguza mguu ambayo aliumia hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages