Breaking News

Your Ad Spot

Aug 28, 2010

KAMPENI UCHAGUZI MKUU

CHADEMA wadaiwa kuzusha tafrani za kutaka kumdunda mtangazaji wa TBC 1.

Uzindunzi wa kampeni za chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) leo katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, umeingia
dosari baada ya wafuasi wa chama hicho kutaka kumpiga mtangazaji wa TBC1, Marin Hassan Marin.
   Habari kutoka viwanja vya Jangwani, zilisema kwamba, katika mkutano huo uliohutubiwa na viongozi mbalimbali akiwemo mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Dk. wilbroad Slaa (pichani akihutubia mkutano huo), wafuasi wa Chadema wanadaiwa ukumvamia mtangazaji huyo na kumtia msuokosuko baada ya kukatishwa ghafla matangazo ya mkutano huo yaliyokuwa yakirushwa moja akwa moja 'live' na kituo hicho.
     Akizungumzia katika taarifa ya habari saa saa 2 usiku huu, Mkurigenzi wa TBC, Tido Mhando alisema, kituo kililazimika kukatiza matangazo hayo kutokana na baadhi ya viongozi kuanza kutoa maneno ya kukashifu mtu binafsi badala ya kunadi sera.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages