Breaking News

Your Ad Spot

Jan 5, 2011

ASSOSA NA MBAZIGWA HASSAN KUUNGURUMA JUMAMOSI HII KATIKA KIPINDI CHA' KAVASHA TIME'

Kipindi hiki ni moja ya vipindi adimu katika Radio, ambacho hurushwa na Mtangazaji Mbazigwa Hassan (Pichani) akishirikiana na mkongwe wa muziki nchini mwenye asili ya Congo-DRC,  Tshimanga Kalala Assossa 'Papaa Tshim'.
    Akizungumza na Chachandu Daily leo, mtayarishaji wa kipindi hicho kaka Mbazigwa, au Mzee wa Kavasha, amesema, Jumamosi hii, anatarajia kuwa na mamabo mazito wakati wa kipindi hicho kitakachoanza saa 11 aflajiri hadi saa 3.00 asubuhi.
    Katika kipindi hicho wasikilizaji watapa fursa ya kutafsiriwa  moja ya nyimbo za Kilingala, ambapo Jumamosi hii, itaendelea tafsiri ya wimbo  'Antention na Sida' wa TP Ok Jazz ulioimbwa na bendi hiyo chini ya Marehemu Franco Lwambo Lwanzo Makiadi. Pia mtangazaji atakuletea mazungumzo na wanamuziki mbalimbali wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao wapo ndani ya nchi hiyo na nje kama Paris, Ivory Coast, Uingereza  na kwamba wanamuziki maarufu waliopo nje ni kama Profesor Vatta Mombasa 'Jujumen' ambaye yupo nchini Ivory Coast na Nzaya  Nzayadyo aliyepo Uingereza  na   na Nyboma  Mwandido ambao w aliwahi kupigia Lipua Lipua katika miaka ya 70,  ambapo viliporomoshwa vibao kama 'Kinzengenzenge' na 'Andoya'.
    Ili kuwa karibu na kupata uhondo huu, fungua  94.6  TBC FM kwa wale wa Dar  es Salaam, Pwani na Zanzibar

1 comment:

  1. mkuu twashukuru sana kutupa taarifa hiz. tutakuwepo Insha-Allah

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages