Breaking News

Your Ad Spot

Jan 25, 2011

MAADALIZI TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA MWAKA HUU YAIVA: KURINDIMA FEBRUARI 9-13 NDANI YA MJIMKONGWE ZENJI.

MKURUGENZI wa Busara Promotions, Yusuf Mahmoud, akizungumza na waandishi wa habari, mjini Dar es Salaam, leo,  kuhusu maandalizi ya Tamasha la Sauti za Busara, ambalo mwaka huu litafanyika Februari 9-13 nadji ya Mjimkongwe,  Zanzibar. kushoto ni Brian Karokola wa Kampuni ya Zanztel inayodhamini tamasha hilo, na kulia ni Mwenyekiti wa maadalizi ya tamasha hilo, Waziri Ally.                                        ===================================

                               STORI
SAUTI za Busara ni moja ya matamasha yenye mvuto wa kipekee barani Afrika, mwaka huu litarindima tena ikiwa ni mara ya nane Visiwani Zanzibar katika Mji Mkongwe kuanzia tarehe 9-13 mwezi ujao.
        Tamasha hili hukutanisha watu wa tanaduni mbalimbali na kuwaweka pamoja, wakisherehekea na kufahamiana kama alivyosema Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake wa ufunguzi wa lamasha la mwaka jana.
        'tukio hili ni muhimu kwa kuwa linatoa fursa kwa wageni na wenyeji wa tanaduni mbalimbali kubadilishana mawazo, kuonyeshana upekee wao, utajiri na utofauti wa muziki wetu. kwa ujumla linachangia kuimarisha muingiliano wa atanaduni na urafiki," alisema Rais Kikwete.
        Sauti za Bisara huwakutanisha wakubwa wa muziki barani Afrika na kuibua vipaji vingine nchini. Mwaka huu vikundi 40 vitatumbuiza, baadhi ni Orchestre poly Ryhmo de Cotonou (Benin),, Blick Bassy (Cameroon), Otentikk Street Brothers (Mauritius), African Stars Band -Twanga Pepeta (Tanzania), Mlimani Park Orchestra (Tanzania), Kwani Experience (Afrika Kusini) na Cultural Musical Club (Zanzibar).
       Nyingine ni Mohammed Ilyas &Nyota Zameremeta ft. Bi Kidude (Zanzibar), Jangwa Music(Tanzania), Bismilahi Garger (Kenya), Maulidi ya Homu ya Mtendeni (Zanzibar), Djeli Moussa Diawara (Guinea) Christine Salem (Reunion),  Yaaba Funk (UK), Muthoni The Drummer Queen (Kenya), jahazi Modern Taarab  (Tanzania),  Les Freres Sissoko (Senegal), Sukiafrika Sukiyaki Allstars (Pan Africa/Far East), GROOVE Lele (Re uinion),  Vusa Mkhaya & Band (Zimbabwe/Various), Djaaka (Musumbiji), Nomakanjani Arts (Zambia), Percussion Discussion Afrika (Uganda), Tunaweza Band (Tanzania), Staff Band namasabo (Tanzania) Lelelele Africa (Kenya), Atemi & The Ma3 band (Kenya) na Sauda (Tanzania).
         Kwa mujibu wa uongozi wa Busara Promotions, sherehe za mwaka huu zitafungwa na maonyesho mbalimbali ya kuvutia, muziki wenye nakshi mbalimbali ikiwemo nyimbo za kiswahili, madansa, maonyesho ya vipande vya filamu za muziki kutoka Tanzania, Uganda, DRC, Ivory Coast na Senegal.
       Wakati huohuo, tamasha litadhamini, Busara Xtra, yaani matukio ya nje ya tamasha yatakayoandakliwa ndani ya zanzibar na ambayo yatawavutia na kuwanufaisha wageni waalikwa.
      Hii itatoa fursa kwa wasanii wa ndani kuonyesha kazi zao, kuwahamasisha wageni kuendelea kutazama maeneo mengine ya visiwa na kuongezakipato kwa watu wengi.

        Vipe vile watu 25 wanatarajiwa kunufaika kwa kupata mafunzo ya kitaaluma ya sauti (live sound engineeing), jukwaa na sanaa ya habari.

*Kwa habari zaidi peruzi katika www.busaramusic.org

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages