Breaking News

Your Ad Spot

Mar 22, 2011

MAJERUHI WA FIVE STARS TAARAB WAFIKA DAR

Baadhi ya majeruhi wa Kundi la Muziki wa Taarab la Five Stars, wakiwa eneo la Equator Grill, Mtoni kwa Azizi Ally, Temeke Dar es Salaam, leo mchana baada ya kufikishwa wakitokea hospitali kuu ya mkoa wa Morogoro. Equator Grill ndiyo ngome kuu ya kundi hilo. (Picha kutoka Isaamichuzi Blog)
============================
Kutoka Morogoro
Picha ya chini ni Mwanamuziki maarufu na mkongwe wa muziki wa taarab, Mwanahawa Ali wa kundio hilo,  akiwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro leo asubuhi baada ya kupatiwa matibabu kutokana na majeraha aliyopata katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria na wasanii wenzake wa Kundi la muziki wa taarab la Five Stars, eneo la Doma, Mikumu nje kidogo ya mji wa Morogoro ambapo wanamuziki 13 waliokuwa katika gari hilo wamekufa papo hapo. (Picha kwa hisani ya mdau wa Morogoro).


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages