Breaking News

Your Ad Spot

Mar 23, 2011

PROF MWANDOSYA ATEMBELEA TBL MWANZA

Waziri wa Majii, Profesa Mark Mwandosya (kulia) Meneja wa Kiwanda cha TBL Mwanza, Richmond Raymond (kushoto) pamoja na Meneja Ubora wa Bidhaa wa kiwanda hicho, Caroline Nhonoli (katikati) alipotembelea hivi karibuni kiwanda hicho kuona uzalishaji wa bia na juhudi mbalimbali za utunzaji na udhibiti wa matumizi ya maji ambayo ni muhimu kwa maisha ya kila siku ya Watu. Ziara hiyo ilikuwa ni moja ya shamrashamra za maadhimisho ya Wiki ya Maji iliyofikia kilele juzi jijini Mwanza.5289
Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya (kulia) akitembelea Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) cha Mwanza, alipofanya ziara hivi karibuni katika kiwanda hicho kuona uzalishaji wa bia na juhudi mbalimbali za utunzaji na udhibiti wa matumizi ya maji ambayo ni muhimu kwa maisha ya kila siku ya Watu. Ziara hiyo ilikuwa ni moja ya shamrashamra za maadhimisho ya Wiki ya Maji iliyofikia kilele juzi jijini Mwanza.
Meneja wa Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Mwanza, Richmond Raymond (mbele kushoto) akimuongoza Waziri wa Majii, Profesa Mark Mwandosya kutembelea mradi wa maji alipofanya ziara hivi karibuni kiwandani hapo, kujionea utendaji wa kiwanda hicho pamoja na mradi huo wa maji unaowahudumia bure wananchi wanaoishi karibu na kiwanda hicho. Ziara hiyo ilikuwa ni moja ya shamrashamra za maadhimisho ya Wiki ya Maji iliyofikia kilele juzi jijini Mwanza..(Picha zote na Mpigapicha maalum)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages