Breaking News

Your Ad Spot

Apr 15, 2011

KATIBU WA WIZARA YA USTAWI WA JAMII, VIJANA, WANWAKE NA WATOTO ZANZIBAR AZIKWA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto)na Makamo wa Rais wa Tanzania, Dk Mohamed Gharib Bilali,(watatu kushoto)  wakijumuika na waislamu wengine kumsalia  Marehemu Rahma Mshangama,aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa jamii,maendeleo ya Vijana Wanawake na Watoto,katika msikiti wa Mwembe Shauri Mjini Zanzibar leo.
Wananchi na waislamu wakiubeba mwili wa Marehemu Rahma Mshangama,aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa jamii,maendeleo ya Vijana Wanawake na Watoto,na kuzikwa makaburi ya Mwanakwerekwe Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akitia udongo katika  kaburi la Marehemu Rahma Mshangama,aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa jamii,maendeleo ya Vijana Wanawake na Watoto,aliyezikwa jana katika makaburi ya mwanakwerekwe mjini Unguja.(Picha zote na Ikulu, Zanzibar)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages